-
Jinsi Tulivyokuja Kujulikana Kuwa Mashahidi wa YehovaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
“Ili hali yetu ipate kujulikana, na kwa sababu ya kuamini kwamba hii inapatana na mapenzi ya Mungu, kama yanavyoelezwa katika Neno lake, NA IAZIMIWE kama ifuatavyo:
“KWAMBA, sisi tunampenda sana Ndugu Charles T. Russell kwa ajili ya kazi yake, na kwamba tunatambua kwa furaha kwamba Bwana alimtumia na kubariki sana kazi yake, lakini hatuwezi kupatana na Neno la Mungu kukubali kuitwa kwa jina ‘Warusselli’; kwamba Watch Tower Bible and Tract Society na International Bible Students Association na Peoples Pulpit Association ni majina tu ya mashirika tuliyo nayo kama kampuni ya Wakristo, nasi twayasimamia na kuyatumia kuendesha kazi yetu kwa kutii amri za Mungu, hata hivyo hakuna lolote la majina hayo linaloambatana nasi wala kutuhusu vya kufaa kutumiwa tukiwa jamii ya Wakristo wanaofuata hatua za Bwana na Bwana-Mkubwa wetu, Kristo Yesu; kwamba sisi tu wanafunzi wa Biblia, lakini tukiwa jamii ya Wakristo walio shirika, tunakataa kujitwalia au kuitwa kwa jina ‘Wanafunzi wa Biblia’ au majina mengine kama hayo ili kutambulisha hali yetu halisi mbele za Bwana; twakataa kuchukua au kuitwa kwa jina la binadamu yeyote;
“KWAMBA, kwa kuwa tulinunuliwa kwa damu yenye thamani ya Yesu Kristo Bwana na Mkombozi wetu, aliyehesabiwa kuwa mwadilifu na kuzaliwa na Yehova Mungu na kuitwa kwenye ufalme wake, bila kusitasita twatangaza ushikamano na ujitoaji wetu wote kwa Yehova Mungu na ufalme wake; kwamba sisi tu watumishi wa Yehova Mungu walioagizwa kufanya kazi kwa jina lake, na kwa kutii amri yake, tutoe ushuhuda wa Yesu Kristo, na kujulisha watu kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli na Mweza Yote; kwa hiyo kwa furaha tunalikubali na kulichukua jina ambalo kinywa cha Bwana Mungu kimelitaja, nasi twataka tujulikane na kuitwa kwa jina hili, yaani, mashahidi wa Yehova [Jehovah’s witnesses].—Isa. 43:10-12, NW.”e
-
-
Jinsi Tulivyokuja Kujulikana Kuwa Mashahidi wa YehovaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
“Tukiwa mashahidi wa Yehova kusudi letu moja tu na la pekee ni kuwa watiifu kabisa kwa amri zake; kujulisha kwamba yeye pekee ndiye Mungu Mweza Yote na wa kweli; kwamba Neno lake ni la kweli na kwamba jina lake lastahili heshima na utukufu wote; kwamba Kristo ni Mfalme wa Mungu, ambaye yeye amemweka juu ya kiti cha ufalme cha mamlaka; kwamba ufalme wake sasa umekuja, na katika kutii amri za Bwana lazima sisi tujulishe sasa habari njema hizi kuwa ushuhuda au ushahidi kwa mataifa na kuarifu watawala na watu juu ya tengenezo katili na lenye uonevu la Shetani, na hasa kwa habari ya ‘Jumuiya ya Wakristo,’ ambayo ndiyo sehemu yenye uovu zaidi ya tengenezo hilo lionekanalo, na juu ya kusudi la Mungu la kuharibu hivi karibuni tengenezo la Shetani, tendo hilo kuu litafuatwa upesi na Kristo Mfalme akiletea vikundi vyote vya watu watiifu wa dunia amani na ufanisi, uhuru na afya, furaha na uhai wa milele; kwamba ufalme wa Mungu ndilo tumaini la ulimwengu, hakuna jingine, na kwamba ujumbe huu lazima utolewe na wale wanaotambulishwa kuwa mashahidi wa Yehova.
“Kwa unyenyekevu twaalika watu wote ambao wamejitoa kabisa kwa Yehova na ufalme wake wajiunge katika kupigia wengine mbiu ya habari hizi njema, ili viwango vyenye uadilifu vya Bwana viinuliwe juu, na kwamba watu wa ulimwengu wapate kujua mahali pa kupata kweli na tumaini kwa ajili ya kitulizo; na zaidi ya yote, kwamba lile jina kuu na takatifu la Yehova Mungu lipate kutetewa na kutukuzwa.”
Si katika Colombus, Ohio, katika Marekani tu, bali kufika mbali sana Australia kwamba wasikilizaji walipiga makofi ghafula waliposikia tangazo la jina hilo jipya. Katika Japani, baada ya saa nyingi za jitihada, ni kisehemu kifupi tu cha programu kilichonaswa katika redio ya masafa mafupi katika usiku wa manane. Mara hiyo kikatafsiriwa. Hivyo kile kikundi kidogo cha huko kilisikia azimio hilo na kishindo cha makofi. Matsue Ishii alikuwapo pamoja nao, na kama alivyoandika baadaye, ‘waliinua kilio cha shangwe kupatana na ndugu zao katika Marekani.’ Kufuatia kusanyiko katika Columbus, makusanyiko na makutaniko ya Mashahidi wa Yehova katika nchi zote ambako walikuwa wakiendeleza huduma yao wajionyesha wenyewe kuwa wakubaliana kabisa na azimio hilo. Kutoka Norway, ikiwa kielelezo kimoja, ilikuja ripoti hii: “Kwenye mkusanyiko wetu wa mwaka . . . katika Oslo sisi sote tuliinuka kwa miguu yetu na kwa idili kubwa tuliinua sauti ‘Ndiyo,’ tulipokuwa tukikubali jina letu jipya ‘mashahidi wa Yehova.’”
-