Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 uku. 5
  • Utangulizi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utangulizi
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Utangulizi

Utangulizi

BIBLIA TAKATIFU ni ufunuo kutoka kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ulioandikiwa watu wote katika dunia hii. Kitabu hiki kilichoongozwa na roho ya Mungu kinavutia watu duniani kote, kwa kuwa kina habari njema za Ufalme wa Mungu, ambao utasimamisha amani na uadilifu. Dunia itakuwa paradiso kwa ajili ya watu wote. Biblia inaonyesha kwamba kwa upendo Mungu aliandaa wokovu kutoka kwenye kifo kwa ajili ya ulimwengu wa wanadamu wenye dhambi, naye alifanya hivyo kupitia dhabihu ya fidia ya Mwana wake, Yesu Kristo.—Yohana 3:16.

Mwanzoni Biblia iliandikwa katika Kiebrania, Kiaramu (lugha yenye uhusiano na Kiebrania), na Kigiriki. Kwa kuwa ni watu wachache leo ambao wanaelewa lugha hizo, imekuwa lazima Biblia Takatifu itafsiriwe katika lugha za kisasa ili kuutangaza ujumbe wake unaotokeza uzima kwa watu wa mataifa yote.

Tafsiri hii mpya ya Biblia ya Kiswahili inategemea chapa ya Kiingereza ya New World Translation of the Holy Scriptures ya mwaka wa 1984. Ina vitabu 39 vya Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu na tafsiri iliyorekebishwa ya Kiswahili ya vitabu 27 vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo iliyochapishwa 1996. Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya iliamua sehemu hizo mbili za Maandiko Matakatifu ziitwe kwa majina ya lugha za kwanza ambazo zilitumiwa kuandika sehemu hizo badala ya kutumia majina yanayotumiwa kwa ukawaida “Agano la Kale” na “Agano Jipya.” Hiyo ni kwa sababu kwa kweli Biblia ni kitabu kimoja tu, na hakuna sehemu iliyopitwa na wakati, au kuwa ya “kale.” Ujumbe wake unapatana kuanzia kitabu cha kwanza cha sehemu ya Kiebrania mpaka kitabu cha mwisho cha sehemu ya Kigiriki. Ili kumsaidia msomaji katika funzo lake la Biblia nzima, tumetia ndani marejeo zaidi ya 125,000 na fahirisi ya baadhi ya maneno ya Biblia.

Kwa kuwa Biblia hueleza mapenzi matakatifu ya Bwana Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote, kuliondoa au kulificha jina la pekee la Mungu, ambalo linapatikana waziwazi mara 7,000 hivi katika maandishi ya Kiebrania, ni ukosefu mkubwa wa heshima, na jambo hilo kwa kweli ni kuukaidi utukufu na mamlaka yake. Kwa hiyo, jambo linalotokeza zaidi katika tafsiri hii ni kule kulirudisha jina la Mungu mahali pake panapofaa katika maandishi ya Biblia. Jambo hilo limefanywa kwa kutumia jina “Yehova” ambalo linakubalika na wengi katika Kiswahili, mara 6,973 katika Maandiko ya Kiebrania na mara 237 katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Ili kupata habari zaidi kuhusu jina hilo, tazama sehemu ya Nyongeza ya tafsiri hii.

Watafsiri wa kitabu hiki, ambao wanampenda Mungu aliye Mtungaji wa Maandiko Matakatifu, wanatambua kwamba wana wajibu wa pekee kwake wa kupitisha mawazo na matangazo yake kwa usahihi kadiri inavyowezekana. Wanatambua pia kwamba wana wajibu kwa wasomaji wanaofanya uchunguzi, ambao wanaitegemea tafsiri ya Neno lililoongozwa na roho ya Mungu Aliye Juu Zaidi kwa ajili ya wokovu wao wa milele. Tunatumaini kwa unyoofu kwamba kwa msaada wa tafsiri hii, msomaji ataweza kuipata njia inayoongoza kwenye uzima usio na mwisho katika ulimwengu mpya wenye uadilifu wa Mweza-Yote.—Isaya 65:17; 2 Petro 3:13.

—Wachapishaji

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki