-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
“Niambie, Mwaka 1975 Wamaanisha Nini?”
Mashahidi walikuwa wameshiriki kwa muda mrefu imani ya kidini ya kwamba Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo ungefuata baada ya miaka 6,000 ya historia ya kibinadamu. Lakini ni lini miaka 6,000 ya kuwako kwa kibinadamu ingekoma? Kitabu Uzima wa Milele—Katika Uhuru wa Wana wa Mungu (Kiingereza), kilichotolewa kwenye mfululizo wa mikusanyiko ya wilaya iliyofanywa katika 1966, kilielekeza kwenye 1975. Humohumo mkusanyikoni, ndugu walipokuwa wakichunguza yaliyomo, kitabu hicho kipya kilizusha mazungumzo mengi juu ya 1975.
Kwenye mkusanyiko uliofanywa katika Baltimore, Maryland, F. W. Franz alitoa hotuba ya kumalizia. Alianza kwa kusema: “Kabla tu ya kufika jukwaani kijana mmoja alinijia na kusema, ‘Niambie, mwaka 1975 wamaanisha nini?’” Ndipo Ndugu Franz aliporejezea maswali mengi ambayo yalizuka juu ya kama habari iliyokuwa katika hicho kitabu kipya ilimaanisha kwamba kufikia 1975 Har–Magedoni ingekuwa imekwisha, na Shetani angefungwa. Yeye alitaarifu, kwa msingi hivi: ‘Ingeweza kuwa. Lakini sisi hatusemi hivyo. Mambo yote yawezekana kwa Mungu. Lakini sisi hatusemi hivyo. Na yeyote wenu asiseme jambo lolote hususa ambalo litatukia kati ya sasa na 1975. Lakini jambo kubwa kati ya yote hayo ni hili, marafiki wapendwa: Wakati ni mfupi. Wakati unakwisha, hakuna shaka juu ya hilo.’
Katika miaka iliyofuata 1966, wengi kati ya Mashahidi wa Yehova walitenda kupatana na maana ya shauri hilo. Hata hivyo, taarifa nyinginezo zilitangazwa juu ya habari hii, na yaelekea nyingine kati yazo zilikuwa dhahiri zaidi ya ilivyopasa kuwa. Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1980 (kurasa 6-7) lilikiri jambo hilo. Lakini Mashahidi wa Yehova walitahadharishwa pia wakazie fikira kufanya mapenzi ya Yehova na wasihangaishwe kupita kiasi na tarehe na matarajio ya wokovu wa mapema.h
-
-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
h Kwa kielelezo, makala zifuatazo zilitangazwa katika Mnara wa Mlinzi: “Kuutumia Wakati Ubakio kwa Hekima” (Julai 1, 1969 au Mei 1, 1968, Kiingereza); “Tumikia kwa Tumaini la Umilele” (Desemba 15, 1974 au Juni 15, 1974, Kiingereza); “Sababu Hatukuambiwa ‘Siku Ile na Saa Ile’” na “Wewe Unahusikaje kwa Kutojua ‘Siku Ile na Saa Ile’?” (Novemba 1, 1975 au Mei 1, 1975, Kiingereza). Mapema zaidi, katika 1963, kitabu “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa,” kilikuwa kimetaarifu hivi: “Hakuna faida kutumia kronolojia ya Biblia kufanya udhanifu [kukisia] juu ya tarehe ambazo zingali za wakati ujao katika mkondo wa wakati.—Mt. 24:36.”
-