-
Kuthamini Wanawake na Kazi YaoAmkeni!—1998 | Aprili 8
-
-
Afya. Ukiwa mama, wahitaji kujitunza, hasa ikiwa u mjamzito au wanyonyesha. Je, waweza kuboresha ulaji wako? Karibu thuluthi mbili za wanawake wajawazito katika Afrika vilevile kusini na magharibi mwa Asia wanaugua kutokana na upungufu wa damu. Mbali na kukumaliza nguvu, upungufu wa damu huongeza hatari zinazohusiana na kuzaa na hufanya iwe rahisi kushambuliwa na malaria. Ingawa nyama na samaki zaweza kuwa zapatikana kwa shida au ni ghali, mayai na mboga au matunda yenye wingi wa chuma yaweza kupatikana. Usiruhusu mapokeo yakuzuie usile vyakula vyenye lishe, wala usiruhusu desturi za kwenu zikuzuie usipate sehemu ya chakula cha familia.b
-
-
Kuthamini Wanawake na Kazi YaoAmkeni!—1998 | Aprili 8
-
-
b Katika nchi nyingine, mapokeo hushikilia kwamba wanawake hawapaswi kula samaki, mayai, au kuku wakati wa ujauzito, kwa kuogopa kumwumiza mtoto asiyezaliwa bado. Wakati mwingine desturi hudai kwamba mwanamke ale chakula kilichobakia, mara baada ya wanaume na wavulana wanapomaliza kula.
-