Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Panama

      Mwalimu wa mazoezi ya mwili anayeitwa Ramiro alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova mnamo 2004. Wakati huo, wanafunzi ambao alipaswa kuzoeza walihitaji saa 12 tu za mazoezi kwa juma ilhali alipaswa kufanya kazi kwa saa 24 kwa juma. Kwa hiyo, msimamizi wa shule alimwambia kwamba atahitaji kutumia muda uliobaki kufundisha wanafunzi hao mambo ya kidini. Msimamizi huyo alimwambia: “Waeleze tu kuhusu Mungu, Yesu, na Biblia.” Ramiro aliwafundisha mambo ambayo alikuwa akijifunza. Mwaka huo, akitumia kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, aliwafundisha wanafunzi 150, waliokuwa katika darasa la sita mpaka nane. Mwaka uliofuata, kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilipotolewa, Ramiro alikuwa amefanya maendeleo na kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa. Aliendelea kufundisha na wakati huu alitumia kitabu Biblia Inafundisha. Wanafunzi walikuwa wameongezeka kufikia 160 wakiwa wamegawanywa katika vikundi sita tofauti. Matokeo yamekuwa nini? Ramiro pamoja na wahubiri wengine katika kutaniko sasa wanajifunza Biblia na wanafunzi kadhaa. Baadhi ya wazazi wao wamethamini kazi ya Ramiro kwa sababu ya mwenendo mzuri wa watoto wao. Wazazi fulani hata wamehudhuria mikutano ya kutaniko na makusanyiko fulani. Ramiro alibatizwa mnamo Novemba 2006 na anatumia kila nafasi anayopata kufundisha kweli za Biblia.

  • Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 50]

      Ramiro akiwa na kitabu “Biblia Inafundisha”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki