-
Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya AjabuSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
KURA YA DANIELI NA YAKO KATIKA PARADISO!
23, 24. (a) Ulimwengu ambao Danieli atajikuta ndani yake utakuwaje tofauti na ulimwengu alioujua? (b) Je, Danieli atakuwa na mahali katika Paradiso, nasi twajuaje?
23 Danieli atataka kujua juu ya ulimwengu atakaojikuta ndani yake wakati huo—ulimwengu ulio tofauti sana na ule alioishi. Hakutakuwa na vita vyovyote wala uonezi wowote ambao uliharibu ulimwengu alioujua. Hakutakuwa majonzi yoyote, ugonjwa wowote, wala kifo chochote. (Isaya 25:8; 33:24) Lakini kutakuwa na wingi wa chakula, nyumba nyingi, na kazi yenye kuridhisha kwa watu wote. (Zaburi 72:16; Isaya 65:21, 22) Wanadamu watakuwa familia moja iliyoungana na yenye furaha.
24 Ni dhahiri kwamba Danieli atakuwa na mahali katika ulimwengu huo. “Utasimama katika kura yako,” malaika alimwambia. (Italiki ni zetu.) Neno la Kiebrania ambalo latafsiriwa “kura” hapa ndilo lilelile ambalo hutumiwa kurejezea viwanja halisi vya shamba.c Huenda Danieli aliujua unabii wa Ezekieli juu ya kugawa nchi iliyorudishwa ya Israeli. (Ezekieli 47:13–48:35) Katika utimizo wake kwenye Paradiso, unabii wa Ezekieli wadokeza nini? Kwamba watu wote wa Mungu watakuwa na mahali katika Paradiso, hata nchi itagawanywa kwa utaratibu na kwa haki. Bila shaka, kura ya Danieli katika Paradiso itahusisha mengi zaidi ya nchi tu. Itatia ndani fungu lake katika kusudi la Mungu huko. Hakika Danieli atapata thawabu aliyoahidiwa.
25. (a) Ni matazamio gani ya maisha katika Paradiso yanayokupendeza? (b) Kwa nini twaweza kusema kwamba Paradiso ni makao ya wanadamu?
25 Hata hivyo, vipi juu ya kura yako? Wewe vilevile waweza kupata ahadi hizo. Yehova anataka wanadamu watiifu ‘wasimame’ kwa ajili ya kura zao, wawe na mahali katika Paradiso. Hebu wazia! Kwa kweli, lingekuwa jambo lenye kusisimua kwelikweli kukutana na Danieli ana kwa ana, pamoja na wanaume na wanawake wengine waaminifu wa nyakati za Biblia. Kisha kutakuwa na wengine wengi watakaofufuliwa, watakaohitaji kufundishwa ili wapate kumjua na kumpenda Yehova Mungu. Jiwazie ukitunza makao yetu ya kidunia na kusaidia kuyafanya yawe paradiso yenye unamna-namna mwingi na uzuri wenye kudumu. Wazia kufundishwa na Yehova, kujifunza kuishi alivyokusudia wanadamu waishi. (Isaya 11:9; Yohana 6:45) Naam, una mahali katika Paradiso. Ingawa huenda wengine wakaiona Paradiso kuwa kitu kipya, kumbuka kwamba mwanzoni Yehova alikusudia wanadamu waishi mahali pa aina hiyo. (Mwanzo 2:7-9) Katika maana hiyo, Paradiso ndiyo makao ya asili ya mabilioni ya wakazi wa dunia. Huko ndiko kwao. Kufikia Paradiso kutakuwa sawa na kurudi nyumbani.
-
-
Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya AjabuSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
c Neno hilo la Kiebrania lahusiana na neno “kijiwe cha mviringo,” kwa kuwa vijiwe vidogo vilitumiwa kupiga kura. Nyakati nyingine nchi iligawanywa hivyo. (Hesabu 26:55, 56) Kichapo A Handbook on the Book of Daniel chasema kwamba hapa neno hilo lamaanisha “kilichowekwa kando (na Mungu) kwa ajili ya mtu.”
-