-
Yehova Amehesabu “Nywele Zenyewe za Kichwa Chenu”Mnara wa Mlinzi—2005 | Agosti 1
-
-
4. Paulo alihitaji kuvumilia hali gani yenye kuendelea, na hali kama hiyo inaweza kutuathiri kwa njia zipi?
4 Fikiria kisa cha mtume Paulo. Aliandika hivi: “Nilipewa mwiba katika mwili, malaika wa Shetani, aendelee kunipiga kofi.” Kisha akaongeza hivi: “Mara tatu nilimsihi Bwana kwamba huo uniondoke.” Yehova alisikia maombi yake. Hata hivyo, alimwonyesha Paulo kwamba hangetatua tatizo lake kimuujiza. Badala yake, Paulo angehitaji kutegemea nguvu za Mungu ili zimsaidie kuvumilia “mwiba katika mwili” wake.b (2 Wakorintho 12:7-9) Kama Paulo, huenda unakabili jaribu fulani lenye kuendelea. Huenda ukawaza hivi, ‘Kwa kuwa inaonekana kwamba Yehova hajaondoa jaribu langu, je, inawezekana kwamba yeye hajui hali yangu au hanijali?’ Jibu ni hapana!
-
-
Yehova Amehesabu “Nywele Zenyewe za Kichwa Chenu”Mnara wa Mlinzi—2005 | Agosti 1
-
-
b Biblia haitaji ‘mwiba ambao Paulo alikuwa nao katika mwili.’ Huenda alikuwa na tatizo fulani la afya, labda macho yake hayakuona vizuri. Au huenda maneno “mwiba katika mwili” yakamaanisha mitume wa uwongo na wengine ambao walipinga huduma na utume wa Paulo.—2 Wakorintho 11:6, 13-15; Wagalatia 4:15; 6:11.
-