-
Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” YetuMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
8. (a) Ni nini ambacho ua wa ndani wa hekalu la kimaono ulikosa? (b) Makuhani kwenye hekalu la kimaono wangejisafisha kwa njia gani?
8 Faida moja ya aina hiyo ni msimamo safi mbele za Yehova. Katika hekalu hilo la kimaono, ua wa ndani unakosa kitu fulani ambacho kilitokeza sana katika ua wa tabenakulo na katika hekalu la Solomoni—beseni kubwa, ambayo baadaye iliitwa bahari, kwa ajili ya makuhani kuogea ndani. (Kutoka 30:18-21; 2 Mambo ya Nyakati 4:2-6) Je, makuhani katika hekalu la kimaono la Ezekieli wangetumia nini kusafishia? Naam, kijito kile cha kimwujiza kinachotiririka kupitia ua wa ndani! Ndiyo, Yehova angewabariki kwa kuwawezesha kufurahia msimamo safi, au mtakatifu.
9. Ni jinsi gani watiwa-mafuta na umati mkubwa waweza kuwa na msimamo safi leo?
9 Vivyo hivyo leo, watiwa-mafuta wamebarikiwa kwa kupewa msimamo safi mbele za Yehova. Yehova huwaona kuwa watakatifu, akiwatangaza kuwa waadilifu. (Waroma 5:1, 2)
-
-
Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” YetuMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
Katika Israeli lililorudishwa, Yehova aliwabariki watu wake kwa mafundisho ya Kimaandiko kupitia ukuhani. (Ezekieli 44:23) Kwa njia kama hiyo, Yehova amewabariki watu wake leo kwa mafundisho tele juu ya Neno lake la kweli, kupitia ule “ukuhani wa kifalme.” (1 Petro 2:9) Ujuzi juu ya Yehova Mungu, juu ya makusudi yake kwa wanadamu, na hasa juu ya Yesu Kristo na Ufalme wa Kimesiya umetiririka kwa wingi unaozidi kuongezeka daima wakati huu wa siku za mwisho. Burudisho la mbubujiko wa kiroho tunaopata na ambao unazidi kuongezeka ni tukufu jinsi gani!—Danieli 12:4.
-