Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Atoa “Fidia Katika Kubadilishana kwa Ajili ya Wengi”
    Mkaribie Yehova
    • 15. Kwa nini ilikuwa lazima Yesu ateseke na kufa?

      15 Katika masika ya mwaka wa 33 W.K., Yesu Kristo alijitolea kuteseka ili alipe fidia. Alijiruhusu kukamatwa kwa mashtaka ya uwongo, kuhukumiwa kuwa na hatia, na kupigiliwa misumari kwenye mti wa mateso. Je, ilikuwa lazima Yesu apatwe na mateso hayo makali? Ndiyo, kwa sababu suala la uaminifu wa watumishi wa Mungu lilihitaji kuamuliwa. Mungu hakumruhusu Herode amwue Yesu akiwa mtoto mchanga. (Mathayo 2:13-18) Lakini akiwa mtu mzima, Yesu aliweza kuvumilia mashambulizi makali ya Shetani akiwa na ujuzi kamili wa masuala yaliyohusika.b Yesu alithibitisha waziwazi kwamba Yehova ana watumishi wanaobaki waaminifu chini ya majaribu kwa sababu ajapoteswa vibaya sana, aliendelea kuwa “mwaminifu-mshikamanifu, asiye na hila, asiyetiwa unajisi, aliyetengwa na watenda-dhambi.” (Waebrania 7:26) Ndiyo sababu kabla tu ya kufa, Yesu alipaaza kilio kwa ushindi: “Imetimizwa!”—Yohana 19:30.

  • Yehova Atoa “Fidia Katika Kubadilishana kwa Ajili ya Wengi”
    Mkaribie Yehova
    • b Ili kufutilia mbali dhambi ya Adamu, Yesu alilazimika kufa akiwa mtu mzima mkamilifu wala si mtoto mkamilifu. Kumbuka kwamba Adamu alitenda dhambi kimakusudi, alijua vizuri kabisa ubaya na matokeo ya tendo lake. Kwa hiyo, ili kuwa “Adamu wa mwisho” na kufunika dhambi hiyo, Yesu alihitaji kuamua kudumisha uaminifu wake kwa Yehova kupatana na ujuzi aliokuwa nao. (1 Wakorintho 15:45, 47) Kwa hiyo, maisha ya Yesu ya uaminifu akiwa duniani kutia ndani kifo chake cha dhabihu yalikuwa “tendo moja la kutetewa kuwa haki.”—Waroma 5:18, 19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki