Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • ‘Kumtandika Yule Bi Kizee’

      Katika miaka ya 1930, ujumbe ambao Mashahidi hawa wenye bidii walipigia mbiu ulitia ndani kufunua wazi dini bandia. Chombo chenye kusaidia katika habari hii kilitolewa kwenye mkusanyiko wa watu wote wa Mashahidi wa Yehova, Septemba 15-20, 1937, katika Columbus, Ohio.

      Jumamosi, Septemba 18, kufuatia hotuba yake ya asubuhi, Ndugu Rutherford alitoa kitabu chenye rangi-hudhurungi Enemies. Kilishutumu dini bandia kuwa “adui mkubwa, sikuzote akidhuru wanadamu.” Wanadini bandia walitambuliwa kuwa “mawakili wa Ibilisi, wawe wanajua hivyo au la.” Alipokuwa akitoa kitabu hicho kwa wasikilizaji, Ndugu Rutherford alisema hivi: “Mtaona kwamba jalada lacho ni rangi-hudhurungi, na kwa kukitumia sisi tutamtandika yule bi kizee.”h Wasikilizaji walikubali kwa sauti kuu na kwa idili.

      Kwa miaka kadhaa gramafoni (kinanda) ilikuwa imetimiza sehemu katika ‘kumtandika yule bi kizee.’

  • Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • “Genge la Wateka-Nyara”

      Upinzani wenye nguvu imara ulitoka kwa vikundi fulani vya Aksio ya Katoliki. Oktoba 2, 1938, Ndugu Rutherford alisema waziwazi sana alipotoa mhadhara “Ufashisti au Uhuru,” ambao baadaye ulitokea kwa namna ya kijitabu na kugawanywa kwa mamilioni. Ndugu Rutherford katika hotuba yake alieleza kirefu visa kadhaa vya matendo ya kuvunja sheria kuonyesha njama iliyofanywa kati ya maofisa fulani wa umma na wawakilishi wa Kanisa la Katoliki ya Roma.

      Baada ya kutoa mambo ya hakika, Rutherford alisema hivi: “Wakati watu wanapoambiwa mambo ya hakika juu ya umati unaotenda kwa kisingizio cha kidini ili kuiba haki zao, Makasisi hupiga yowe na kusema: ‘Uwongo! Wekeni kizibo vinywani mwao na msiwaruhusu kusema.’” Ndipo akauliza: “Je, ni kosa kutangaza kweli kuhusu genge la wateka-nyara wanaonyang’anya watu? Hasha! . . . Je, watu wanyoofu wazibwe vinywa na kushurutishwa kukaa kimya huku genge hili la wateka-nyara likiharibu uhuru mbalimbali wa watu? Zaidi ya yote, je, watu wanyimwe mapendeleo yao waliyopewa na Mungu ya kukusanyika kwa amani na uhuru wa ibada ya Mungu Mweza Yote, na uhuru wa kusema kuhusu ufalme wake na wale wanaoupinga?”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki