Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • David Souris alitumwa Le Port,

  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kikundi cha tatu kilianzishwa katika jiji lenye bandari la Le Port mwanzoni mwa miaka ya 1960, na kilitia ndani watu wenye kupendezwa kutoka Saint-Paul, mji ulio umbali wa kilomita nane hivi kusini ya Le Port. Jiji la Le Port lilikuwa na nyumba za mbao zilizokuwa na ua wa mmea fulani aina ya dungusi usio na miiba. David Souris alikodi nyumba na kuanza kufanya mikutano humo. Mnamo Desemba 1963, ndugu waliomba kikundi chao kiwe kutaniko. Wahubiri wa Ufalme walikuwa 16, na 8 kati yao walikuwa wamebatizwa. Walihubiri wastani wa saa 22.5 kila mwezi. David pamoja na msaidizi wake waliongoza mafunzo 38 ya Biblia! Mwangalizi wa mzunguko alipowatembelea mwezi huo, alitoa hotuba iliyosikilizwa na watu 53.

      Mapainia wa pekee Christian na Josette Bonnecaze walitumwa Le Port pia. Christian aliyebatiziwa Guiana ya Ufaransa alikuja Réunion mapema miaka ya 1960. Wakati huo alikuwa mseja, na katika familia yao hakuna mwingine aliyekuwa Shahidi. Kwa fadhili, Ndugu Souris alihamia nyumba nyingine ili Christian na mke wake Josette wakae katika nyumba iliyokuwa inatumiwa kwa ajili ya mikutano. Lakini baada ya muda, kutaniko hilo lilikua sana mpaka wenzi hao wakalazimika kuhama pia!

      Wakati huo makasisi katika eneo hilo lililokuwa na Wakatoliki wengi walianza kuwachochea watu wawachukie Mashahidi. Mara nyingi vijana waliwarushia wahubiri mawe mchana. Usiku waliyarusha juu ya paa za nyumba za akina ndugu.

      Mwanafunzi mpya wa Biblia Raphaëlla Hoarau aliwajua baadhi ya vijana hao. Pindi moja baada ya vijana hao kurusha mawe, mwanafunzi huyo aliwafuata nyumbani kwao na kuwaambia: “Mkiendelea kumrushia ndugu yangu mawe, nitawaonyesha cha mtema kuni.”

      “Pole sana Bi. Hoarau. Hatukujua huyo ni ndugu yako,” wakasema.

      Raphaëlla na mabinti wake watatu walikubali kweli na mmoja wao, Yolaine, akaolewa na Lucien Véchot.

      Ijapokuwa makasisi waliwachochea watu wachukie Mashahidi, kutaniko lenye bidii lilianzishwa Le Port kwa sababu ndugu walikuwa wenye bidii na Mungu aliwabariki. Muda si mrefu, jumba walilofanyia mikutano lilijaa pomoni. Mara nyingi walio wengi walisikiliza wakiwa nje. Viti viliwekwa kila mahali, hata jukwaani, na watoto fulani waliketi ukingoni mwa jukwaa wakitazama wasikilizaji. Hatimaye, ndugu walijenga Jumba la Ufalme zuri, na sasa eneo hilo lina makutaniko sita.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki