Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Lucien Véchot akatumwa jijini Saint-André,

  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Katika mwaka uliotangulia, ndugu huko Saint-André waliomba kikundi chao kiwe kutaniko. Barua yao ilisema: “Mwishoni mwa Juni 1963, tutakuwa na wahubiri 12 waliobatizwa, na katika miezi miwili ijayo, inawezekana tutakuwa na wahubiri wapya 5 au 6. Ndugu wanaongoza mafunzo 30 ya Biblia.” Ombi lao lilikubaliwa, na kutaniko hilo likasimamiwa na ndugu wawili—Jean Nasseau aliyekuwa mtumishi wa kutaniko, au mwangalizi msimamizi, na Lucien Véchot msaidizi wake. Wote walikuwa wamebatizwa kwa muda usiozidi miaka miwili.

      Jean mwenye umri wa miaka 38, alikuwa mtu mkubwa, mwenye fadhili, na mkarimu. Alikuwa pia mjenzi stadi aliyefundisha katika shule fulani ya ufundi. Alibatizwa 1962 na alikuwa na uwezo wa kuwachochea watu waendeleze kazi ya Ufalme. Hata aligharimia ujenzi wa Jumba la Ufalme la pili kisiwani Réunion lililojengwa kwenye kiwanja chake huko Saint-André. Jengo hilo lililojengwa kwa mbao lilikuwa thabiti na lenye kuvutia, na lilitoshea vizuri zaidi ya watu 50. Makutaniko manane yameanzishwa katika eneo hilo ambalo mwanzoni lilihubiriwa na kikundi cha Saint-André. Jean alikufa akiwa mwaminifu kwa Yehova mwaka wa 1997.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki