-
Réunion2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kwa mfano, mjini Saint-Louis, ndugu fulani kijana alikuwa akijifunza kazi ya uashi wakati kutaniko lilipopokea ramani ya ujenzi ya Jumba la Ufalme. Ndugu huyo alimhubiria mwalimu wake, akamweleza kuhusu jumba hilo, na kumjulisha kuwa litajengwa na wafanyakazi wa kujitolea. Mwalimu huyo alifanya nini? Aliwaleta wanafunzi kwenye ujenzi ili wapate mazoezi ya kujenga! Walisaidia kuchimba msingi, na baadaye mwalimu huyo akachanga vyuma vya kujengea msingi huo.
Ndugu waliamua kutengeneza bamba la sementi lenye ukubwa wa mita 190 za mraba wakati wa sikukuu. Wafanyakazi wa kujitolea zaidi ya mia moja walifika asubuhi na mapema kufanya kazi hiyo. Lakini kwa sababu fulani, maji yalikuwa yamefungwa mjini! Ndugu mmoja aliyemjua mkuu wa zimamoto alimweleza tatizo hilo, na mara moja mkuu huyo mwenye fadhili akatuma gari la zimamoto likiwa na maji ya kutosha kwa kazi hiyo.
Jumba la Ufalme lilipokamilika, mtu aliyekuwa ameanza kujifunza Biblia karibuni na aliyevutiwa na ndugu na kazi yao, alichukua kitabu chake cha hundi na kuchanga pesa ambazo karibu zilitosha kununua mfumo mpya wa sauti. Carey Barber wa Baraza Linaloongoza alipotembelea Mauritius mwaka wa 1988, alikuja Réunion ili kutoa hotuba ya kuweka jumba hilo wakfu.
-
-
Réunion2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 248]
Jumba la Ufalme lililojengwa Saint-Louis mnamo 1988
-