Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Katika mwaka uliotangulia, ndugu huko Saint-André waliomba kikundi chao kiwe kutaniko. Barua yao ilisema: “Mwishoni mwa Juni 1963, tutakuwa na wahubiri 12 waliobatizwa, na katika miezi miwili ijayo, inawezekana tutakuwa na wahubiri wapya 5 au 6. Ndugu wanaongoza mafunzo 30 ya Biblia.” Ombi lao lilikubaliwa, na kutaniko hilo likasimamiwa na ndugu wawili—Jean Nasseau aliyekuwa mtumishi wa kutaniko, au mwangalizi msimamizi, na Lucien Véchot msaidizi wake. Wote walikuwa wamebatizwa kwa muda usiozidi miaka miwili.

  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Makutaniko manane yameanzishwa katika eneo hilo ambalo mwanzoni lilihubiriwa na kikundi cha Saint-André.

  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mnamo Desemba 1963, ndugu waliomba kikundi chao kiwe kutaniko. Wahubiri wa Ufalme walikuwa 16, na 8 kati yao walikuwa wamebatizwa. Walihubiri wastani wa saa 22.5 kila mwezi. David pamoja na msaidizi wake waliongoza mafunzo 38 ya Biblia! Mwangalizi wa mzunguko alipowatembelea mwezi huo, alitoa hotuba iliyosikilizwa na watu 53.

      Mapainia wa pekee Christian na Josette Bonnecaze walitumwa Le Port pia. Christian aliyebatiziwa Guiana ya Ufaransa alikuja Réunion mapema miaka ya 1960. Wakati huo alikuwa mseja, na katika familia yao hakuna mwingine aliyekuwa Shahidi. Kwa fadhili, Ndugu Souris alihamia nyumba nyingine ili Christian na mke wake Josette wakae katika nyumba iliyokuwa inatumiwa kwa ajili ya mikutano. Lakini baada ya muda, kutaniko hilo lilikua sana mpaka wenzi hao wakalazimika kuhama pia!

  • Réunion
    2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ijapokuwa makasisi waliwachochea watu wachukie Mashahidi, kutaniko lenye bidii lilianzishwa Le Port kwa sababu ndugu walikuwa wenye bidii na Mungu aliwabariki. Muda si mrefu, jumba walilofanyia mikutano lilijaa pomoni. Mara nyingi walio wengi walisikiliza wakiwa nje. Viti viliwekwa kila mahali, hata jukwaani, na watoto fulani waliketi ukingoni mwa jukwaa wakitazama wasikilizaji. Hatimaye, ndugu walijenga Jumba la Ufalme zuri, na sasa eneo hilo lina makutaniko sita.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki