Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwekwa Huru na Kweli
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Februari 1
    • Alipokuwa na umri wa miaka 17, Markietta alipata fursa bora kabisa ya kuzungumza na wengine darasani mwake juu ya imani yake. “Tulipewa mgawo wa kutoa hotuba,” yeye asema. “Nilichagua habari yangu iwe juu ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.a Nilichagua sura tano kutoka hicho kitabu, nikaandika vichwa vyazo kwenye ubao wa kuandikia. Niliomba darasa liorodheshe vichwa hivyo kulingana na umaana wavyo.” Mazungumzo ya maswali na majibu pamoja na darasa yakafuata. “Nililionyesha darasa hicho kitabu,” Markietta amalizia, “na wanafunzi kadhaa wakaomba kupata nakala. Hata mwalimu wangu alisema kuwa alitaka nakala moja.”

  • Kuwafikia Watu wa Namna Zote na Kweli
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Februari 1
    • ◻ Katika kisiwa kimoja magharibi mwa Pasifiki ambako kazi ya Mashahidi wa Yehova iko chini ya marufuku, mvulana mwenye umri wa miaka 12 alijikuta amezungukwa na mashirika mabaya shuleni. Wengi wa wanadarasa wake walivuta sigareti, walisoma fasihi za kiponografia, waliwasumbua walimu, na kushiriki katika mapigano kwa ukawaida. Hali ilipata kuwa mbaya sana hivi kwamba huyo mvulana alimwomba babake kama angeweza kuhamia shule nyingine. Lakini baba alisababu pamoja na mwanaye dhidi ya wazo hilo, kwa kuwa alihisi kwamba mwenendo wa wanafunzi katika shule nyingine za karibu haungekuwa tofauti. Hata hivyo, angemsaidiaje mtoto wake?

      Huyo baba alikumbuka akiwa na kitabu cha vijana nyumbani. Kilikuwa zawadi kutoka kwa mtu wa ukoo aliyekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo alikitafuta hicho kitabu, na alipokiona, alimpatia mwanaye. Kichwa chacho kilikuwa Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi.a Huyo mvulana aliipata sura “Naweza Kukabilianaje na Msongo wa Marika?” kuwa yenye kusaidia hasa. Haikumfunza umuhimu wa kudumisha hali ya kujistahi tu bali ilimfunza pia jinsi ya kusema la kwa busara wakati wengine walipojaribu kumsonga afuate mwendo usio wa hekima. Kwa kutumia kanuni za Kimaandiko zipatikanazo ndani ya hicho kitabu, huyo mwanamume kijana alijifunza jinsi ya kukabiliana kwa mafanikio na msongo wa marika.

      Kwa kuona mabadiliko hayo chanya na mengine katika mwanaye, baba aliamua kukisoma hicho kitabu. Akipendezwa na mashauri yenye kutumika yapatikanayo ndani ya hicho kitabu, baba aliomba Mashahidi wa Yehova funzo la Biblia nyumbani. Baadaye washiriki wengine wa familia yake walijiunga naye katika hilo funzo. Tokeo likawa nini? Huyo mvulana, ndugu yake mchanga, babake, na babu na nyanya yake sasa ni Mashahidi wa Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki