-
Viumbe Wana Hisi za AjabuAmkeni!—2003 | Machi 8
-
-
Uwezo wa Kuhisi Umeme
Kisa kilichotajwa mwanzoni kuhusu samaki aina ya wayo na papa kilitukia wakati wa uchunguzi wa kisayansi kuhusu papa. Watafiti walitaka kujua iwapo papa na samaki aina ya taa wanaweza kuhisi nguvu kidogo za umeme zinazotokezwa na samaki aliye hai.c Walipitisha kiasi kinachofaa cha umeme kwenye mabamba yaliyowekwa mchangani katika kidimbwi chenye papa. Ikawaje? Mara tu papa alipoyakaribia mabamba hayo, aliyashambulia vikali.
Papa wanaweza kuhisi nguvu za umeme kama vile sikio linavyoweza kusikia sauti mbalimbali. Lakini, samaki wengine hutokeza nguvu za umeme. Kama vile popo anavyotoa mlio na kusikiliza mwangwi wake, samaki hao hutokeza mawimbi ya umeme, kisha wakitumia vipokezi maalumu wanaweza kutambua jinsi mawimbi hayo yanavyobadilika yanapogonga kitu fulani.d Kwa kutumia njia hiyo, samaki hao wanaweza kujua mahali penye vizuizi, windo, au hata mwenzi.
-
-
Viumbe Wana Hisi za AjabuAmkeni!—2003 | Machi 8
-
-
c Viumbe wote walio hai, kutia ndani wanadamu, hutokeza kiasi kidogo cha umeme kinachoweza kutambuliwa wanapokuwa ndani ya maji.
-
-
Viumbe Wana Hisi za AjabuAmkeni!—2003 | Machi 8
-
-
d Samaki tunaozungumzia hapa hutokeza nguvu kidogo sana za umeme. Wao ni tofauti na samaki wengine kama vile taa na mkunga, ambao hutokeza nguvu nyingi za umeme ili kushtua adui au kunasa windo. Mkunga hutokeza nguvu nyingi sana za umeme zinazoweza kumuua farasi!
-
-
Viumbe Wana Hisi za AjabuAmkeni!—2003 | Machi 8
-
-
[Picha katika ukurasa wa 7]
Taa—hutambua nguvu za umeme
[Picha katika ukurasa wa 7]
Kwezi—huona
-