-
‘Utaendelea Kuishi’ Kama Yeremia?Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
9. Ni shauri gani lililoongozwa na roho kuhusu ndoa tunalopaswa kufikiria kwa uzito?
9 Wakristo wengi hufunga ndoa, lakini si wote. Yesu hakufunga ndoa, naye alisema kwamba baadhi ya wanafunzi wake wangekuwa na zawadi ya ‘kuupa nafasi’ useja katika akili na mioyo yao. Aliwahimiza wale ambao wangeweza, wafanye hivyo. (Soma Mathayo 19:11, 12.) Kwa hiyo, ingefaa kumpongeza, wala si kumdhihaki, mtu anayebaki mseja ili kufanya mengi katika utumishi wa Mungu.
-
-
‘Utaendelea Kuishi’ Kama Yeremia?Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
11 Waseja wengi Wakristo—wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee—wanafuata mfano mzuri wa Yeremia. Mambo yaliyoonwa yanaonyesha kwamba kuna faida kubwa kujishughulisha na utumishi wa Mungu na kushiriki kikamili katika utendaji wa kiroho. Kwa mfano, dada mmoja Shahidi anayeshirikiana na kutaniko la Kichina anasema: “Upainia umenipa kusudi maishani. Nikiwa mseja, ninakuwa na shughuli nyingi, mambo mengi ya kufanya, na hivyo sijioni mpweke. Kila siku mimi huhisi nimeridhika ninapoona jinsi huduma yangu inavyowasaidia watu. Hilo hunipa shangwe kubwa.” Painia mwenye umri wa miaka 38 anasema: “Nafikiri siri ya kuwa mwenye furaha ni kuwa na maoni yanayofaa kuhusu hali yoyote ile maishani.” Dada mmoja mseja huko Ulaya Kusini alisema hivi waziwazi: “Maisha yangu hayakwenda nilivyokusudia, hata hivyo, nina furaha nami nitaendelea hivyo.”
12, 13. (a) Tunapaswa kuwa na maoni gani yanayofaa kuhusu useja na ndoa? (b) Maisha na shauri la Paulo yanakazia nini kuhusu useja?
12 Inawezekana kwamba Yeremia aliona kuwa maisha yake hayakwenda alivyotazamia alipokuwa kijana? Huenda alitambua pia kwamba hata kwa wale waliofunga ndoa na kuwa na watoto, mambo hayakwenda walivyotazamia. Dada mmoja painia nchini Hispania alisema: “Najua watu waliofunga ndoa walio na furaha na wengine wasio na furaha. Kujua hilo hunisaidia kuona kwamba furaha yangu haitegemei ikiwa nitafunga ndoa au hapana.” Bila shaka, kutokana na kisa cha Yeremia na wengine wengi, ni wazi kwamba mseja anaweza kuwa na maisha mazuri, yenye kuridhisha, na yenye furaha. Maneno ya Paulo pia yanathibitisha hilo: “Sasa nawaambia waseja na wajane, ni vema kwao wabaki kama mimi nilivyo.” (1 Kor. 7:8) Huenda Paulo alikuwa mjane. Vyovyote vile, alikuwa mseja alipokuwa na shughuli nyingi katika utumishi wa umishonari. (1 Kor. 9:5) Je, hudhani kwamba aliweza kutimiza mengi hivyo kwa kuwa alikuwa mseja? Kwake useja ulimaanisha “kumhudumia Bwana daima bila kukengeushwa fikira,” na hivyo akatimiza mambo mengi mazuri.—1 Kor. 7:35.
-