Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Ujiweke Wakfu kwa Yehova?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
    • Kumbuka kwamba kwa sababu ya dhambi ya Adamu, sote tumezaliwa nje ya familia ya Mungu. (Rom. 3:23; 5:12) Kujiweka wakfu kwa Mungu ni takwa la maana sana ili tukubaliwe katika familia yake ya ulimwenguni pote. Hebu tuone kwa nini hilo ni takwa la maana.

      11 Hakuna yeyote kati yetu aliyezaliwa na baba ambaye angeweza kumpitishia uhai ambao Mungu alikusudia tuwe nao—uhai mkamilifu. (1 Tim. 6:19) Hatukuzaliwa tukiwa wana wa Mungu kwa sababu wenzi wawili wa kwanza walipofanya dhambi, jamii yote ya wanadamu ilitengwa mbali na Baba yao mwenye upendo, Muumba wao. (Linganisha na Kumbukumbu la Torati 32:5.) Kuanzia wakati huo na kuendelea, wanadamu wamekuwa wakiishi nje ya familia ya Yehova ya ulimwenguni pote, wakiwa wametengwa mbali na Mungu.

      12. (a) Wanadamu wasio wakamilifu wanaweza jinsi gani kuwa washiriki wa familia ya Mungu? (b) Ni lazima tuchukue hatua gani kabla ya kubatizwa?

      12 Hata hivyo, kila mmoja wetu anaweza kumwomba Mungu amruhusu ajiunge na familia Yake ya watumishi ambao amewakubali.a Hilo linawezekana jinsi gani kwa watenda-dhambi kama sisi? Mtume Paulo aliandika hivi: “Tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kupitia kifo cha Mwana wake.” (Rom. 5:10) Tunapobatizwa tunatoa ombi kwa Mungu la kupata dhamiri njema ili tuweze kukubalika kwake. (1 Pet. 3:21) Hata hivyo, kabla ya kubatizwa kuna hatua ambazo tunapaswa kuchukua. Ni lazima tumjue Mungu, tujifunze kumwamini, tutubu, na kubadili njia zetu. (Yoh. 17:3; Mdo. 3:19; Ebr. 11:6) Na kuna jambo lingine ambalo linahitajiwa ili tukubaliwe katika familia ya Mungu. Ni jambo gani hilo?

      13. Kwa nini ni jambo linalofaa kwa mtu kuweka nadhiri ya wakfu kwa Mungu ili awe sehemu ya familia Yake ya waabudu anaowakubali?

      13 Ili mtu ambaye ametengwa mbali na Mungu aweze kuwa mshiriki wa familia ya Mungu ya watumishi anaowakubali, anahitaji kwanza kutoa ahadi rasmi mbele za Yehova. Ili kuelewa kwa nini anahitaji kufanya hivyo, hebu fikiria baba mwenye heshima anayemjali sana kijana yatima. Baba huyo angependa kumchukua kijana huyo ili awe mshiriki wa familia yake. Baba huyo anajulikana kuwa mtu mzuri. Hata hivyo, kabla ya kumkubali kijana huyo kuwa mwana wake, anataka kijana huyo atoe ahadi. Kwa hiyo, anasema, “Kabla sijakubali uwe mwana wangu, ninataka kujua ikiwa utanipenda na kuniheshimu nikiwa baba yako.” Atakubali kijana huyo ajiunge na familia yake ikiwa tu kijana huyo yuko tayari kutoa ahadi hiyo rasmi. Takwa hilo linapatana na akili, sivyo? Vivyo hivyo, watu ambao Yehova anakubali wajiunge na familia yake ni wale tu ambao wako tayari kuweka nadhiri ya kujiweka wakfu kwake. Biblia inasema hivi: “Jitoeni ninyi wenyewe kwake: dhabihu iliyo hai, iliyo wakfu na ambayo anaweza kukubali.”—Rom. 12:1, The New English Bible.

  • Kwa Nini Ujiweke Wakfu kwa Yehova?
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 15
    • a “Kondoo wengine” wa Yesu wataweza tu kuwa wana wa Mungu mwishoni mwa miaka elfu moja. Hata hivyo, kwa kuwa wamejiweka wakfu kwa Mungu, kwa kufaa wanaweza kumwita Mungu “Baba,” na wanaweza kuonwa kuwa washiriki wa familia ya waabudu wa Yehova.—Yoh. 10:16; Isa. 64:8; Mt. 6:9; Ufu. 20:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki