-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
Ingawa katika mfano mwingine Yesu anatuambia kwamba mbegu ambayo inapandwa ni “neno la ufalme,” katika mfano huu, anatuambia kwamba mbegu hiyo nzuri inafananisha jambo lingine tofauti, inafananisha “wana wa ufalme.” (Mt. 13:19, 38) Hao si raia wa Ufalme bali ni “wana,” au warithi wa Ufalme.—Rom. 8:14-17; soma Wagalatia 4:6, 7.
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
4. (a) Mtu anayetajwa katika mfano huo ni nani? (b) Yesu alianza wakati gani na jinsi gani kupanda mbegu hiyo?
4 Mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake ni nani? Yesu anajibu swali hilo baadaye anapowaeleza hivi wanafunzi wake: “Mpandaji wa mbegu nzuri ni Mwana wa binadamu.” (Mt. 13:37) Yesu, ambaye ni “Mwana wa binadamu,” alitayarisha shamba katika kipindi cha miaka mitatu na nusu ya huduma yake duniani ili apande mbegu. (Mt. 8:20; 25:31; 26:64) Kisha kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K. na kuendelea, alianza kupanda mbegu nzuri, yaani, “wana wa ufalme.” Inaonekana kwamba mbegu hiyo ilipandwa wakati Yesu, akiwa mwakilishi wa Yehova, alipoanza kuwamwagia wanafunzi wake roho takatifu, na hivyo akawatia mafuta ili wawe wana wa Mungu.b (Mdo. 2:33)
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
b Katika mfano huo, kazi ya kupanda mbegu haifananishi kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, ambayo ingewakusanya watu wapya ambao wangekuwa Wakristo watiwa-mafuta. Yesu alisema hivi kuhusu mbegu nzuri ambayo inapandwa katika shamba: “Hiyo ni [si kwamba “itakuwa”] wana wa ufalme.” Kupanda kunafananisha kuwatia mafuta wana hao wa Ufalme katika shamba la ulimwengu.
-