Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Kurudishwa Upesi Sana na kwa Ghafula

      13. “Sauti ya fujo” ni nini katika utimizo wa kwanza?

      13 Isaya anatoa unabii hivi: “Sauti ya fujo itokayo mjini! Sauti itokayo hekaluni! Sauti ya BWANA awalipaye adui zake adhabu!” (Isaya 66:6)

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 14. (a) Malaki alitabiri nini kuhusu kuja kwa Yehova kwenye hekalu Lake? (b) Kulingana na unabii wa Ezekieli, matokeo yalikuwa nini Yehova alipokuja kwenye hekalu lake? (c) Yehova na Yesu walilichunguza hekalu la kiroho wakati gani, na matokeo yakawa nini kwa wenye kudai eti wanawakilisha ibada safi?

      14 Maneno haya katika Isaya yanapatana na matamko mengine mawili ya kiunabii. Tamko moja ni lile lililoandikwa kwenye Ezekieli 43:4, 6-9 na lile jingine liko kwenye Malaki 3:1-5. Ezekieli na hata Malaki wanautabiri wakati ambao Yehova Mungu anakuja kwenye hekalu lake. Unabii wa Malaki unaonyesha kwamba Yehova anakuja kuchunguza nyumba yake ya ibada safi na kutenda kama Mtakasaji, akiwakataa wale wanaomwakilisha vibaya. Njozi ya Ezekieli inaonyesha Yehova akiingia katika hekalu na kudai kwamba alama zote za ukosefu wa adili na za ibada ya sanamu ziondolewe.b Katika utimizo wa kisasa wa unabii huo mbalimbali, jambo muhimu la kiroho lilitokea mwaka wa 1918 kuhusiana na ibada ya Yehova. Ushuhuda unaonyesha kwamba Yehova na Yesu waliwachunguza wale wote wale waliodai kuwakilisha ibada safi. Matokeo ya uchunguzi huo ni kwamba, mwishowe Jumuiya ya Wakristo yenye ufisadi ilitupiliwa mbali. Uchunguzi huo ulitokeza kipindi kifupi cha kuwatakasa watiwa-mafuta wa Kristo, kisha wakarudishiwa upesi sana hali nzuri ya kiroho mwaka wa 1919.—1 Petro 4:17.

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 15. Ni uzazi gani unaotabiriwa, na unatimizwaje mwaka wa 537 K.W.K.?

      15 Hali hiyo ya kurudishwa inaonyeshwa kwa kufaa sana katika mistari ifuatayo ya Isaya: “Kabla hajaona utungu alizaa; kabla maumivu yake hayajampata, alizaa mtoto mwanamume. Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara? Maana Sayuni, mara alipoona utungu, alizaa watoto wake.” (Isaya 66:7, 8)

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 16. Katika utimizo wa kisasa wa Isaya 66:7, 8, Sayuni inafananisha nini, na wazao wake wamezaliwaje upya?

      16 Katika utimizo wa kisasa, Sayuni inawakilisha “mwanamke” wa kimbingu wa Yehova, yaani tengenezo lake la kimbingu la viumbe-roho. Mwaka wa 1919 “mwanamke” huyu alishangilia kuona kuzaliwa kwa wana wake watiwa-mafuta duniani ili wawe watu waliopangwa kitengenezo, maana yake “taifa.” Tukio hilo la kuzaliwa upya lilifanyika upesi sana, tena kwa ghafula.c Katika muda wa miezi michache tu, watiwa-mafuta wakiwa kikundi walitoka katika hali ya kutotenda iliyo kama kifo, wakaanza maisha ya utendaji wa kujibidiisha sana katika “nchi” yao, yale makao yao ya utendaji wa kiroho waliyopewa na Mungu. (Ufunuo 11:8-12) Kufikia miezi ya mwishoni mwa mwaka wa 1919, hata walitangaza kuchapishwa kwa gazeti jipya la kukamilishana na Mnara wa Mlinzi. Kichapo hicho kipya kiliitwa The Golden Age (sasa Amkeni!), na kilikuwa ushuhuda wa kwamba watu wa Mungu wametiwa nguvu mpya, wakiwa wamepangwa tena kuwa tengenezo kwa ajili ya utumishi.

      17. Yehova anawahakikishiaje watu wake kwamba hakuna cha kumzuia asitimize kusudi lake kuhusiana na Israeli wa kiroho?

      17 Katika ulimwengu mzima hakuna nguvu yoyote ambayo ingeweza kuzuia uzaliwa huo mpya. Mstari unaofuata unasema lilo hilo: “Je! mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? asema BWANA; mimi nizalishaye, je! nilifunge tumbo? asema Mungu wako.” (Isaya 66:9) Sawa na vile hatua za kuzaa mtoto zisivyoweza kuepukwa zikiisha kuanza, ndivyo kuzaliwa upya kwa Israeli wa kiroho hakungeweza kuzuiliwa baada ya kuanza. Ni kweli kwamba upinzani ulikuwako, na yaelekea kwamba kutakuwako upinzani zaidi wakati ujao. Lakini ni Yehova peke yake aliye na uwezo wa kukomesha kitu anachokianzisha. Hata hivyo, yeye hafanyi hivyo kamwe! Ingawa hivyo, Yehova anawatendeaje watu wake waliotiwa nguvu mpya?

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • c Uzaliwa unaotajwa hapa kwa njia ya unabii sio ule ule unaoelezwa kwenye Ufunuo 12:1, 2, 5. Katika sura hiyo ya Ufunuo, “mwana, wa kiume,” anafananisha Ufalme wa Kimesiya, ulioanza kazi mwaka wa 1914. Hata hivyo, “mwanamke” wa unabii anayetajwa katika maandiko hayo mawili ni yule yule.

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Utunzaji Mwororo wa Yehova

      18, 19. (a) Yehova anatumia mfano gani wenye kugusa moyo, nao unatumikaje kuwahusu watu wake walio uhamishoni? (b) Leo mabaki watiwa-mafuta wamefaidikaje na lishe na utunzaji wenye upendo?

      18 Mistari minne inayofuata inaufafanua utunzaji mwororo wa Yehova kwa njia ya kuvutia. Kwanza, Isaya anasema hivi: “Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake.” (Isaya 66:10, 11) Hapa Yehova anatumia mfano wa mwanamke anayenyonyesha kitoto chake kichanga. Mtoto mchanga anapoumwa na njaa, kazi yake ni kulia-lia tu. Lakini anapoletwa karibu na matiti ya mama yake anyonye, sasa yeye huacha kihoro chake na kutosheka akiwa na furaha kamili.

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 19 Israeli wa kiroho pia alibarikiwa kwa lishe tele baada ya kurudishwa mwaka wa 1919. Tangu wakati huo, chakula cha kiroho kinachotolewa kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kimekuwa kikitiririka kwa ukawaida. (Mathayo 24:45-47) Kweli huu umekuwa wakati wa faraja na shangwe kwa mabaki watiwa-mafuta. Lakini kumekuwako na baraka nyingine nyingi.

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 20. Yerusalemu limebarikiwaje kwa “kijito kifurikacho,” nyakati za kale na za kisasa pia?

      20 Unabii unaendelea kusema hivi: “BWANA asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa [“ubavuni,” “NW”]; na juu ya magoti mtabembelezwa.” (Isaya 66:12) Hapa mfano wa kunyonyesha umeunganishwa na wazo la mtiririko wa baraka nyingi, yaani “mto” na “kijito kifurikacho.”

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Hata hivyo, utimizo mkubwa zaidi umetukia wakati wetu wenyewe ambapo “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha”—ambao kwa kweli ni miminiko kubwa sana la wanadamu—wamejiunga na mabaki ya Wayahudi wa kiroho.—Ufunuo 7:9; Zekaria 8:23.

  • Yehova Hubariki Ibada Safi
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 23. Simulia hali yenye furaha ya watu wa Yehova waliorudishwa.

      23 Yehova huonyesha upendo wake kwa matendo. Hivyo, yeye anaendelea kusema hivi: “Nanyi mtaona, na mioyo yenu itafurahi, na mifupa yenu itasitawi kama majani mabichi; na mkono wa BWANA utajulikana, uwaelekeao watumishi wake, naye atawaonea adui zake ghadhabu.” (Isaya 66:14) Mtaalamu fulani wa sarufi ya Kiebrania anadokeza kwamba usemi “nanyi mtaona” una wazo la kwamba popote pale ambapo wahamishwa wanaorudi wanatazama katika nchi yao iliyorudishwa, “sasa macho yao yanaona shangwe tupu.” Watashangilia vilivyo, wasisimuke hata midomo ibaki wazi kwa kuona kwamba wamerudishwa kwenye nchi yao kipenzi. Watahisi kurudishiwa nguvu za ujana, kana kwamba mifupa yao imeanza kuimarika tena, wapate nguvu mpya kama nyasi wakati wa masika. Watu wote watajua kwamba hali hii yenye baraka haikutokea kwa jitihada ya mwanadamu yeyote, bali kwamba imesababishwa na ‘mkono wa Yehova.’

      24. (a) Wewe unakata kauli gani unapoyafikiria matukio yanayowahusu watu wa Yehova leo? (b) Tunapaswa kufanya azimio gani?

      24 Je, wewe unatambua wakati mkono wa Yehova unapofanya kazi miongoni mwa watu wake leo? Hakuna mwanadamu yeyote yule ambaye angaliweza kuirudisha ibada safi. Hakuna mwanadamu angaliweza hata kidogo kusababisha mamilioni ya watu wa thamani kubwa wamiminike kutoka katika mataifa yote kujiunga na mabaki waaminifu katika nchi yao ya kiroho. Ni Yehova Mungu peke yake awezaye kufanya hayo. Maonyesho hayo ya upendo wa Yehova yanatupa sisi sababu ya kuwa na shangwe nyingi sana. Tusithubutu kamwe kuuchezea-chezea upendo wa Yehova. Na tuendelee ‘kutetemeka tusikiapo neno lake.’ Na tuazimie kuishi kwa kufuata kanuni za Biblia na kufurahia kumtumikia Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki