-
Alikata “Kauli Moyoni Mwake”Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 1
-
-
Je, Maria angeunga mkono uamuzi wa Yosefu wa kutii amri hiyo? Hiyo ingekuwa safari ngumu kwake. Huenda huo ulikuwa msimu wa mvua ndogo kwa kuwa msimu wa kiangazi ulikuwa ukiisha. Isitoshe, maneno “akapanda kutoka Galilaya” yanafaa, kwa kuwa mji wa Bethlehemu ulikuwa zaidi ya mita 760 juu ya usawa wa bahari. Baada ya kutembea kwa siku kadhaa, huo ungekuwa mwinuko mkubwa sana wenye kuchosha. Huenda safari hiyo ingechukua muda mrefu zaidi kwa kuwa Maria angehitaji kupumzika mara nyingi kwa sababu ya hali yake. Wakati kama huo, huenda mwanamke angetaka kukaa karibu na watu wa familia na marafiki wake ambao wangekuwa tayari kumsaidia wakati ambapo uchungu wa kuzaa ungeanza. Bila shaka, alihitaji kuwa na ujasiri ili asafiri.
Hata hivyo, Luka anaandika kwamba Yosefu alienda “kuandikishwa pamoja na Maria.” Pia anasema kwamba Yosefu ‘alikuwa amemwoa Maria kama ilivyoahidiwa.’ (Luka 2:4, 5) Yosefu alikuwa na uvutano mkubwa sana juu ya maamuzi ya Maria kwa kuwa sasa Maria alikuwa mke wake. Maria alimwona mume wake kuwa kichwa chake kuhusiana na mambo ya kiroho, na alikubali jukumu lake alilopewa na Mungu la kuwa msaidizi wake kwa kuunga mkono maamuzi yake.a Kwa hiyo, alishinda kipingamizi hicho cha imani yake kwa kutii.
Ni nini kingine kilichomchochea Maria atii? Je, alijua unabii wa kwamba Masihi angezaliwa Bethlehemu? Biblia haisemi. Hatuwezi kupuuza uwezekano huo, kwa maana jambo hilo lilijulikana na viongozi wa kidini na watu kwa ujumla. (Mathayo 2:1-7; Yohana 7:40-42) Maria pia aliyajua Maandiko. (Luka 1:46-55) Vyovyote vile, iwe Maria alisafiri ili kumtii mumewe, kutii Kaisari, au kwa sababu ya unabii wa Yehova au iwe alichochewa na mambo hayo yote matatu, aliweka mfano bora. Yehova anathamini sana roho ya unyenyekevu na utii inayoonyeshwa na wanaume na wanawake. Siku hizi ambapo kujitiisha ni mojawapo ya sifa zinazodharauliwa, mfano wa Maria ni kielelezo kizuri kwa watu waaminifu kila mahali.
-
-
Alikata “Kauli Moyoni Mwake”Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 1
-
-
a Ona tofauti kati ya andiko hilo na simulizi la safari ya mapema zaidi: “Maria akaondoka . . . akaenda” kumtembelea Elisabeti. (Luka 1:39) Wakati huo, akiwa mwanamke anayechumbiwa ambaye hakuwa ameolewa, Maria angeweza kusafiri bila kumwuliza Yosefu. Lakini baada ya kuolewa, ingawa walisafiri pamoja inasemekana kwamba Yosefu ndiye aliyefanya uamuzi wa kusafiri, si Maria.
-