-
Unapima Mafanikio Jinsi Gani?Mnara wa Mlinzi—2007 | Januari 1
-
-
Unapima Mafanikio Jinsi Gani?
JESSE LIVERMORE, alionwa na watu fulani kuwa mfanyabiashara aliyefanikiwa zaidi katika soko la hisa la Wall Street. Alijulikana kuwa mtu aliyefanya maamuzi ya kibiashara yenye hekima. Kwa hiyo, alitajirika sana. Alivalia suti nzuri sana zilizoshonwa kwa mikono. Aliishi katika nyumba kubwa yenye vyumba 29, naye alitumia gari jeusi la kifahari aina ya Rolls-Royce na alikuwa na dereva wake.
Davida pia alikuwa ameazimia kufanikiwa. Akiwa msaidizi wa mwenyekiti na meneja mkuu wa kampuni kubwa ya uchoraji, alikuwa akikaribia kuwa msimamizi wa idara fulani ya kampuni hiyo. Alivutiwa sana na utajiri na umaarufu. Hata hivyo, David alifanya uamuzi ambao ulimwongoza ajiuzulu. David alisema hivi: “Ninajua kwamba sitapata tena kazi kubwa kama hiyo.” Je, unafikiri David alikosea?
Watu wengi wanaamini kwamba kufanikiwa ni kupata utajiri, sifa, au umaarufu. Hata hivyo, wale walio matajiri huenda bado wanahisi kwamba maisha yao ni matupu na hayana kusudi. Bwana Livermore alihisi hivyo. Ingawa alikuwa tajiri, maisha yake yalikuwa yenye kuvunja moyo sana, yalijaa misiba na huzuni. Alishuka moyo sana, kila ndoa aliyofunga ilivunjika, naye hakuwa na uhusiano mzuri na watoto wake. Mwishowe, baada ya kupoteza utajiri wake mwingi, siku moja Bwana Livermore aliketi katika baa kwenye hoteli fulani ya kifahari na kujisikitikia kwa sababu ya hasara alizopata. Aliomba kinywaji, akatoa kijitabu chake chenye jalada la ngozi na kumwandikia mke wake barua ya kumuaga. Alipomaliza kinywaji, aliingia katika chumba fulani ambacho hakikuwa na mwangaza wa kutosha, kisha akajiua.
-
-
Jinsi Unavyoweza KufanikiwaMnara wa Mlinzi—2007 | Januari 1
-
-
Kwa mfano, David aliyetajwa mapema, alitarajiwa kufanya kazi kwa saa nyingi zaidi na kufunga safari nyingi za kibiashara. David anasema: “Nilikuwa nikiondoka asubuhi sana siku ya Jumatatu (Siku ya 1) na kurudi Alhamisi (Siku ya 4) jioni.” Wakijua kwamba mtu anahitaji kujidhabihu hivyo, marafiki, washiriki wa familia, na wafanyakazi wanyoofu walimhimiza David hivi: “Fanya hivyo kwa ajili ya familia yako.” Walimwambia angefanya hivyo kwa miaka michache tu mpaka ajiimarishe. David anaeleza hivi: “Walinisadikisha kwamba familia yangu ingefaidika kwa sababu ningeleta pesa zaidi nyumbani na ningefanikiwa zaidi. Ingawa sikuwa pamoja na familia yangu, marafiki wangu walinisadikisha kwamba kwa kweli nilikuwa nikiisaidia.” Kama David, watu wengi wanafanya kazi kwa bidii ili kuipa familia yao kila kitu ambacho wanafikiri wapendwa wao wanahitaji. Lakini je, kufuata mashauri ya aina hiyo kunaleta mafanikio? Familia inahitaji nini hasa?
David aligundua kile ambacho familia yake ilihitaji alipokuwa mbali katika safari ya kibiashara. “Nilipokuwa nikizungumza na binti yangu Angelica kwenye simu, aliniambia hivi: ‘Baba, kwa nini hutaki kukaa nyumbani pamoja nasi?’ Maneno hayo yaliniumiza sana moyoni,” akasema David. Maneno hayo ya binti yake yalimchochea kupeleka ombi lake la kujiuzulu. David aliamua kuipa familia yake kile ambacho walihitaji hasa, yaani, yeye.
-