-
Ugarit—Jiji la Kale Lililokuwa Kwenye Kitovu cha Ibada ya BaaliMnara wa Mlinzi—2003 | Julai 15
-
-
Jiji na maeneo yake tambarare yaliyolizunguka yalijaa mahekalu ya Baali na ya Dagani.b Minara hiyo ya hekalu ambayo huenda ilikuwa na urefu wa meta 20, ilikuwa na ukumbi ulioongoza kwenye chumba cha ndani kilichokuwa na sanamu ya mungu aliyeabudiwa. Kulikuwa na ngazi iliyoongoza juu kwenye sebule ambako mfalme alikuwa akisimamia sherehe mbalimbali. Wakati wa usiku au wakati wa dhoruba, inawezekana kwenye kilele cha mahekalu kulikuwa na milingoti iliyokuwa na mwangaza uliongoza meli kwa usalama mpaka bandarini. Bila shaka, mabaharia ambao waliona kwamba kurudi kwao salama kulitegemea Baali-Hadadi, mungu wa dhoruba, walitoa michango ya nanga za meli 17 ambazo zilipatikana ndani ya hekalu la mungu huyo.
-
-
Ugarit—Jiji la Kale Lililokuwa Kwenye Kitovu cha Ibada ya BaaliMnara wa Mlinzi—2003 | Julai 15
-
-
b Ijapokuwa kuna maoni yanayotofautiana, wataalamu fulani wanatambua hekalu la Dagani kuwa ndilo hekalu la mungu Eli. Roland de Vaux, msomi wa Biblia Mfaransa katika Shule ya Yerusalemu ya Mafunzo ya Biblia, anasema kwamba Dagani, yaani Dagoni wa kitabu cha Waamuzi 16:23 na 1 Samweli 5:1-5 ni jina la kibinafsi la mungu Eli. Kitabu The Encyclopedia of Religion kinatoa maelezo haya: “Dagani alikuwa akishirikishwa au kufananishwa na [Eli].” Katika maandishi ya Ras Shamra, Baali anaitwa mwana wa Dagani, lakini maana ya neno “mwana” hapa si hakika.
-