-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Kwa sababu wewe ulishika lile neno juu ya uvumilivu wangu, mimi pia nitakinga wewe na ile saa ya mtihani, inayopasa kuja juu ya dunia yote kwa ujumla inayokaliwa, ili kuweka mtihani juu ya wale wanaokaa juu ya dunia.
-
-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
16, 17. (a) Ni ipi “ile saa ya mtihani, inayopasa kuja juu ya dunia yote kwa ujumla inayokaliwa”? (b) Hali ya wapakwa-mafuta ilikuwa nini mwanzoni mwa “ile saa ya mtihani”?
16 Hata hivyo, ni ipi “ile saa ya mtihani”? Pasipo shaka, Wakristo hao katika Esia walipaswa wakabiliane na wimbi jingine la mnyanyaso mbaya sana kutoka Roma yenye milki.c Hata hivyo, ule utimizo ulio mkubwa ni ile saa ya kupepeta na kuhukumu ambayo mwishowe iliwasili katika kipindi cha siku ya Bwana, ikifikia upeo tangu 1918 na kuendelea. Ule mtihani umekuwa wa kuamulia kama mmoja anaunga mkono Ufalme wa Mungu uliosimamishwa au ulimwengu wa Shetani. Ni wa kipindi kifupi kwa kulinganisha, “saa” moja, lakini haujakwisha. Mpaka uishe, ni lazima sisi tusisahau kamwe kwamba tunaishi katika “ile saa ya mtihani.”—Luka 21:34-36.
17 Katika 1918 jamii ya Yohana ya Wakristo wapakwa-mafuta—kama kundi hilo mathubuti katika Filadelfia—ilikuwa sharti ikabili upinzani kutoka “sinagogi la Shetani” la ki-siku-hizi. Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, ambao hudai kuwa Wayahudi wa kiroho, waliongoza kwa hila watawala wakandamize Wakristo wa kweli. Hata hivyo, hao walijaribu sana ‘kushika neno la uvumilivu wa Yesu’; kwa sababu hiyo, kwa msaada wa kiroho, “nguvu chache” zenye maana, waliokoka na wakaamshwa waingie kupitia mlango ambao sasa ulifunguliwa mbele yao.
-