-
Wakati Ujao Unaotegemeka!Amkeni!—2008 | Mei
-
-
Jina Unaloweza Kulitegemea!
Kama vile sahihi inavyohalalisha hundi, ndivyo jina la Mungu la kibinafsi, Yehova, linavyoandaa uhakikisho kuhusu ahadi zote zilizorekodiwa katika Biblia.b Mwandikaji wa Biblia ambaye Mungu alimjali kwa upendo mara nyingi alisema hivi: “Tumelitegemea jina lake takatifu.”—Zaburi 33:21; 34:4, 6.
Likihusianisha jina la Mungu na sifa yake akiwa baba mwenye kujali, Methali 18:10 linasema: “Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu. Mwadilifu hukimbilia humo na kupewa ulinzi.” Hali kadhalika, Waroma 10:13 linasema: “Kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.” Bila shaka, jina la kibinafsi la Mungu si hirizi inayomlinda mtu asipatwe na mabaya. Badala yake, Mungu mwenyewe ndiye anayewaokoa, na wale wanaomwitia kama andiko hilo linavyosema wanafanya hivyo kwa sababu wanamtegemea kabisa, wakijua vizuri kwamba kila mara yeye hutimiza ahadi zake. Zaburi 91:14 inasema hivi: “Kwa sababu ameweka upendo wake juu yangu [Yehova], mimi nitamwokoa pia. Nitamlinda kwa sababu amelijua jina langu.”
-
-
Wakati Ujao Unaotegemeka!Amkeni!—2008 | Mei
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 9]
JINA NA UHAKIKISHO
Jina la Mungu, Yehova, si kibandiko tu.c Jinsi gani? Jina hilo linamaanisha “Yeye Husababisha Kuwa.” Kwa maneno rahisi, Mungu ana upendo, nguvu, na hekima ya kuwa chochote anachohitaji kuwa ili kutimiza kusudi na neno lake. Kwa mfano, anaweza kuwa Mwokozi wa waadilifu, Mwangamizaji wa waovu, Msikiaji wa sala, au Baba mwenye upendo—chochote anachochagua kuwa.
“Mimi ni Mungu,” asema Yehova, “Yeye anayetangaza tangu mwanzo ule mwisho . . . Yeye anayesema, ‘Shauri langu mwenyewe litasimama, na kila jambo ambalo ni mapenzi yangu nitafanya.’” (Isaya 46:9, 10) Kwa kuwa nyakati zote Mungu hushikamana na ahadi yake na kwa kuwa jina lake, au sifa yake, inahusika, Neno lake lililoandikwa litatimia hakika. “Mungu si mwanadamu kwamba aseme uwongo.”—Hesabu 23:19.
[Maelezo ya Chini]
c Jina Yehova linatofautiana kabisa na majina ya cheo kama vile Mweza-Yote, Muumba, Mungu, na Bwana. Jina hilo linapatikana mara elfu saba hivi katika maandishi ya awali ya Biblia Takatifu. Mungu alijipa jina hilo. Andiko la Kutoka 3:15 linasema hivi: “Jehova . . . hili ndilo jina langu milele.”—The Old Testament in Swahili (Mombasa).
-