-
“Wema Wake, Jinsi Ulivyo Mwingi!”Mkaribie Yehova
-
-
18. Yehova ni “mwingi wa . . . kweli” katika maana gani, na kwa nini maneno hayo yanatia moyo?
18 “Mwingi wa . . . kweli.” Kusema uwongo ni zoea la kawaida ulimwenguni leo. Lakini Biblia inatukumbusha hivi: “Mungu si mtu, aseme uongo.” (Hesabu 23:19) Isitoshe, andiko la Tito 1:2 linasema kwamba ‘Mungu hawezi kusema uwongo.’ Hawezi kusema uwongo kwa sababu yeye ni mwema sana. Kwa hivyo, ahadi za Yehova zinategemeka kabisa; maneno yake hayawezi kamwe kukosa kutimia. Yehova anaitwa pia “Mungu wa kweli.” (Zaburi 31:5) Mbali na kutosema uwongo, anaeneza ukweli kwa wingi. Yeye hafanyi mambo kwa kujificha au kisirisiri, bali yeye huwafundisha watumishi wake waaminifu hekima yake isiyo na mipaka.b Hata anawafundisha jinsi ya kuishi kupatana na kweli hizo ili ‘waendelee kutembea katika kweli.’ (3 Yohana 3)
-
-
“Wema Wake, Jinsi Ulivyo Mwingi!”Mkaribie Yehova
-
-
b Kwa kufaa, Biblia inaonyesha kwamba kweli inahusiana na nuru. Mtunga-zaburi aliimba hivi: ‘Niletee nuru yako na kweli yako.’ (Zaburi 43:3) Yehova anawaangazia nuru nyingi ya kiroho wale walio na nia ya kufundishwa au kuelimishwa naye.—2 Wakorintho 4:6; 1 Yohana 1:5.
-