-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Tuvalu: Peteli, ambaye jina lake linamaanisha “Betheli,” ni msichana mwenye miaka 14 aliye na tatizo kubwa sana la kusikia. Baadhi ya watu wake wa ukoo ni Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo, hapo awali alihudhuria mikutano kadhaa, lakini hakunufaika sana kwa sababu hakusikia yaliyozungumziwa wala hakujua kusoma. Peteli alijifunza kusoma midomo. Hivi majuzi, dada mmishonari anayeitwa Dale, alianza kujifunza naye kwa kutumia broshua Furahia Milele Maisha Duniani! Dale alitumia picha za broshua hiyo ili kumfundisha Peteli habari za Biblia. Pia alitumia maandishi yake ili kumfundisha kusoma. Jambo hilo lilikuwa gumu hasa kwa sababu Dale ni mmishonari mpya ambaye bado anajifunza lugha, Peteli naye alihitaji kuonyeshwa jinsi ya kutamka maneno ifaavyo. Peteli ana bidii na hamu ya kujifunza. Baada ya miezi mitatu tu alijua kusoma. Yeye na yule dada mmishonari hutayarisha pamoja maelezo kwa ajili ya mikutano. Peteli hufanya mazoezi kwa bidii kabla ya mikutano na hujivunia kutoa maelezo. Yeye huketi mbele katika Jumba la Ufalme ili aone vizuri midomo ya msemaji. Dale anaandika hivi: “Pole kwa pole Yehova amekuwa rafiki wa kweli wa Peteli, naye hutokwa na machozi mara kwa mara tunapoongea kuhusu wakati ambapo ‘masikio ya viziwi yatazibuliwa.’”—Isa. 35:5.
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 57]
Dale na Peteli, Tuvalu
-