Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ripoti ya Ulimwenguni Pote
    2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Samoa: Elena ambaye ni painia anajifunza Biblia pamoja na mwanamke Mmethodisti. Nyumba ya mwanamke huyo ilikuwa karibu na nyumba ya kasisi wa kanisa la eneo hilo. Walikuwa wakijifunzia kwenye sehemu ya nyumba yake ambayo haina ukuta. Kwa hiyo, kasisi huyo aliweza kuwaona. Siku moja walipokuwa wakijifunza, yule kasisi alikuja. Huyo mwanafunzi wa Biblia alimuuliza alichotaka. Kasisi huyo alimjibu: “Ninamtafuta nguruwe wangu mdogo. Sijamwona kwa karibu mwezi mzima.” Kisha akamgeukia Elena na kumuuliza, “Unajua ni kwa nini nguruwe wangu mdogo alitoroka?” Elena alifikiri anaongea kumhusu nguruwe halisi, kwa hiyo akasema kwamba huenda alitoroka kwa sababu alikuwa akimpa chakula kilekile kila siku. Alimpendekezea ampe chakula kingine. Elena alishangaa kasisi huyo alipomwelekezea kidole yule mwanafunzi wa Biblia na kusema, “Huyu ndiye nguruwe wangu mdogo!” Kisha akaongeza: “Wewe umemwiba. Ni lazima mkomeshe funzo hili mara moja na msithubutu kujifunza tena kamwe.” (Makasisi katika vijiji vya Samoa wana mamlaka kubwa.) Mwanamke huyo alilia. Elena alijitahidi kumtuliza na kumweleza kwamba kulingana na Biblia mambo kama hayo yangewapata wale wanaojifunza Biblia.

      Elena alibadili siku, wakati, na mahali pa funzo. Yeye anasema: “Badala ya kujifunza katika sehemu ya nyumba isiyo na ukuta, tulifanyia funzo kwenye chumba kidogo nyuma ya nyumba ya mwanamke huyo. Kulikuwa na joto kali ndani ya chumba hicho lakini angalau tuliweza kuendelea kujifunza. Tulijifunza katika chumba hicho kwa miezi miwili. Halafu siku moja, baada ya sala ya kufungua, yule kasisi aliingia ghafula. Nilifikiri alikuja kusimamisha funzo, lakini mtazamo wake ulikuwa umebadilika.”

      Alijiunga nasi katika funzo na hata akauliza maswali. Baada ya funzo alimgeukia huyo mwanamke na kusema: “Nataka kukuambia jambo fulani. Jana usiku tulienda mjini, lakini tulipokuwa njiani kurudi nyumbani, gari letu liliharibika karibu na kijiji jirani. Mume na mke vijana, na mwanamume mwingine kijana, walikuja kutusaidia kutengeneza gari. Lakini gari lilikataa kuwaka, kwa hiyo, nikaliacha nyumbani kwao nao wakajitolea kutupeleka kwetu. Nilipoingia katika gari lao, niliona magazeti ya Mnara wa Mlinzi na vitabu vingine. Nilifikiri huenda ikawa watu hao ni wafuasi wa kanisa lilelile la mwanamke huyu ambaye hukutembelea.”

      Mwanafunzi wangu alimjibu hivi: “Ni kweli kabisa, wao ni watoto wa Elena.” Aliomba radhi, kisha akasema: “Endelea kujifunza. Sasa najua kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wema na wenye upendo sana. Nisamehe kwa mambo niliyosema hapo awali. Funzo kama hili lingewasaidia wafuasi wa kanisa langu kubadili mitazamo yao.” Kuanzia siku hiyo, badala ya kujifunza katika kile chumba kidogo chenye joto jingi kilicho nyuma ya nyumba hiyo, wamekuwa wakijifunza katika sehemu ya mbele ya nyumba hiyo. Sehemu hiyo ya mbele iliyo wazi haina joto kali. Tangu wakati huo, kasisi hajawasumbua ijapokuwa anaweza kuwaona vizuri wakijifunza.

  • Ripoti ya Ulimwenguni Pote
    2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 58]

      Elena, Samoa

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki