-
Mapendekezo ya Kutoa BroshuaHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Mapendekezo ya Kutoa—Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?
Baada ya kumsalimu mwenye nyumba, unaweza kusema:
“Matatizo na hali zenye kufadhaisha ni za kawaida katika maisha ya leo. Unafikiri maisha yalikusudiwa kuwa hivi? [Mruhusu ajibu.] Broshua hii inaonyesha kwamba kusudi la Mungu kuelekea wanadamu na dunia litatimizwa hatimaye. [Zungumzia picha iliyo kwenye ukurasa wa 20-21. Kisha usome fungu la 9 na ukazie Isaya 14:24 na 46:11.] Nitakaporudi, nitakuonyesha Maandiko yanayosema kwamba Mungu ataifanya dunia iwe Paradiso tena.” Mwachie broshua na upange kurudi.
-
-
Mapendekezo ya Kutoa BroshuaHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Mhubiri kijana anaweza kusema:
“Vijana wengi wa rika langu hawajui maisha yatakuwaje wakati ujao. Unafikiri maisha ya kizazi kinachokuja yatakuwa bora? [Mruhusu ajibu.] Biblia inasema kwamba wanadamu wote watakuwa na wakati ujao mzuri. [Mwonyeshe picha kwenye ukurasa wa 31, na usome maelezo ya picha. Kisha usome 2 Petro 3:13.] Broshua hii inazungumzia baraka ambazo Mungu atawaletea wanadamu. [Kazia vichwa vidogo vyenye herufi nzito kwenye ukurasa wa 29-30, na umtolee broshua hiyo.] Ningependa kurudi tena ili nikuonyeshe ahadi ya Mungu ya kukomesha vita vyote.” Panga kurudi.
-
-
Mapendekezo ya Kutoa BroshuaHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Mtu mzima anapohubiri na mtoto, anaweza kujitambulisha pamoja na mtoto na kusema:
“Ukipenda, ________ anaweza kukuonyesha picha na kusoma andiko moja katika Biblia. [Mtoto amwonyesha picha na kusoma maelezo ya picha kwenye ukurasa wa 31, kisha asome Ufunuo 21:4.] Broshua hii inaeleza hatua ambayo Mungu atachukua kuelekea matatizo tunayokabili leo. [Kazia kwa ufupi vichwa vidogo vyenye herufi nzito kwenye ukurasa wa 29-30, na umtolee broshua.] Tutakaporudi, nitakuonyesha Biblia inasema nini kuhusu mwisho wa matatizo yote ya afya.”
-