Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/05 kur. 3-6
  • Mapendekezo ya Kutoa Broshua

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapendekezo ya Kutoa Broshua
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha
  • Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
  • Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
  • Ni Nini Hutupata Tunapokufa?
  • Je! Uamini Utatu?
  • Furahia Milele Maisha Duniani!
  • Serikali Itakayoleta Paradiso
  • Mapendekezo ya Kutoa—Je! Kweli Mungu Anatujali?
  • **********
  • **********
  • Mapendekezo ya Kutoa—Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?
  • **********
  • **********
  • Broshua kwa Ajili ya Watu wa Dini Zisizo za Kikristo
  • Lasting Peace and Happiness—How to Find Them
  • “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”
  • Why Should We Worship God in Love and Truth?
  • Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?
  • Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
  • Mwongozo wa Mungu —Njia Yetu ya Kwenda Paradiso
Huduma ya Ufalme—2005
km 7/05 kur. 3-6

Tunza

Mapendekezo ya Kutoa Broshua

Nyongeza hii ina mapendekezo mbalimbali ya kukusaidia kutayarisha utangulizi wa kutoa broshua. Mapendekezo hayo yanaweza kubadilishwa ili yafae eneo lenu. angulizi nyingine zinaweza pia kutumiwa. Tangulizi za kutoa broshua ambazo hazijaonyeshwa katika nyongeza hii zinaweza kutayarishwa kwa kutumia mapendekezo hayo.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme, Januari 2005, uku. 8.

Kila dokezo katika ukurasa huu lina (1) swali lenye kuchochea fikira ili kuanzisha mazungumzo, (2) chanzo cha habari katika broshua, na (3) andiko linalofaa ambalo linaweza kusomwa wakati wa mazungumzo. Unaweza kuongezea maneno yako ikitegemea itikio la mtu.

Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha

“Duniani pote, watu wanatafuta maisha bora. Unafikiri itawezekana kweli kupata maisha yenye kuridhisha kabisa?”—uku. 29, fu. 6; 2 Pet. 3:13.

Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote

“Unafikiri mashauri ya Biblia yanafaa leo?”—uku. 22, maelezo ya picha; uku. 23, fu. la 3 katika sanduku; Met. 25:11.

Jina la Mungu Litakaloendelea Milele

“Wengi wetu tunaijua ile sala inayoanza hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe.’ (Mt. 6:9, Union Version) Lakini je, ulijua kwamba ni lazima tulijue jina hilo ili tuokolewe?”—uku. 28, fu. 1; Rom. 10:13.

Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa

“Leo tunawatolea watu broshua hii ambayo imewafariji na kuwapa tumaini mamilioni ya watu ambao wamefiwa na wapendwa wao. Umewahi kujiuliza kuna tumaini gani kwa wafu?”—uku. 27, fu. 3; Yoh. 5:28, 29.

“Umewahi kuwazia jinsi unavyoweza kumfariji mtu aliyefiwa na mpendwa wake?”—uku. 20, fu. 1; Met. 17:17.

Ni Nini Hutupata Tunapokufa?

“Watu tunaowapenda wanapokufa, ni jambo la kawaida kujiuliza wako wapi na kama tutawaona tena. Umewahi kufikiria maswali kama hayo?”—Maswali kwenye jalada la nyuma; Ayu. 14:14, 15.

Je! Uamini Utatu?

“Watu wana maoni mbalimbali kuhusu utu wa Mungu. Unafikiri kile tunachoamini ni muhimu?”—uku. 3, fu. 3, 7-8; Yoh. 17:3.

Furahia Milele Maisha Duniani!

“Watu wengi wanafikiri kwamba lazima waende mbinguni ili wafurahie uzima wa milele, lakini una maoni gani kuhusu kuishi duniani milele?”—Picha kwenye jalada; Ufu. 21:4.

Serikali Itakayoleta Paradiso

“Watu wengi wanatamani kuona matatizo tunayokabili leo yakisuluhishwa. Unafikiri kuna serikali yoyote itakayosuluhisha matatizo haya?”—uku. 3, fu. 1; Mt. 6:9, 10.

Mapendekezo ya Kutoa—Je! Kweli Mungu Anatujali?

Baada ya kutaja msiba fulani uliotokea, unaweza kusema:

“Umewahi kujiuliza kwa nini Mungu huwaacha wanadamu wateseke ikiwa kweli anatujali? [Mruhusu ajibu.] Broshua hii inajibu swali hilo vizuri na inaonyesha mambo ambayo Mungu atafanya hivi karibuni. [Mwonyeshe picha kwenye ukurasa wa 27, kisha usome Zaburi 145:16 katika fungu la 22.] Mungu atakomeshaje mateso yote yanayowakumba wanadamu? Ningependa kuzungumzia swali hilo nitakaporudi.” Mtolee broshua, na upange kurudi.

Unaporudi, unaweza kusema:

“Mara ya mwisho nilipokutembelea, tulisoma andiko hili. [Soma au nukuu Zaburi 145:16.] Kisha niliuliza swali: Mungu atakomeshaje mateso yote yanayowakumba wanadamu?” Mwombe alete broshua yake. Fungua ukurasa wa 27-28, na uzungumzie fungu la 23-25. Muulize kama angependa kujifunza Biblia, au fanya mpango wa kuzungumzia fungu la 26 na 27 katika ziara itakayofuata.

**********

Mhubiri kijana anaweza kusema:

“Vijana wengi wa rika langu wanajiuliza jinsi ulimwengu utakavyokuwa miaka 10 au 15 ijayo. Unafikiri ulimwengu utakuwaje wakati huo? [Mruhusu ajibu.] Matatizo tunayoona leo yanaonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho. [Soma 2 Timotheo 3:1-3.] Broshua hii inajibu maswali haya. [Soma maswali yaliyo kwenye jalada, kisha umtolee broshua.] Ningependa kurudi, ikiwa utakuwa na dakika chache, ili nikuonyeshe habari fulani yenye kutia moyo kuhusu mwisho wa magonjwa na kuzeeka.” Fanya mpango wa kurudi.

Unaporudi, unaweza kusema:

“Mara ya mwisho tulipozungumza, nilikwambia kwamba ningependa kukuonyesha habari yenye kutia moyo kuhusu mwisho wa magonjwa na kuzeeka. Habari hiyo inazungumziwa hapa.” Mwombe alete broshua yake, kisha msome na kuzungumzia fungu la 6-7 kwenye ukurasa wa 23 hadi 24 wa broshua hiyo. Fanya mpango wa kuzungumzia fungu la 8 na 9 kwenye ziara itakayofuata.

**********

Mtu mzima anapohubiri na mtoto, anaweza kujitambulisha pamoja na mtoto huyo na kusema:

“Ukimruhusu, ________ angependa kukusomea andiko moja. [Mtoto anasoma Zaburi 37:29 na kutoa maelezo mafupi.] Broshua hii inazungumzia jinsi Mungu atakavyotimiza kusudi lake kuelekea wanadamu na dunia. [Mwonyeshe picha kwenye ukurasa wa 24-27.] Tutakaporudi, nitakuonyesha ahadi nzuri sana ya Biblia kuhusu ufufuo.” Mtolee broshua, na upange kumrudia.

Mtu mzima anaporudi, anaweza kusema:

“Nilipokutembelea wakati uliopita, tulisoma Zaburi 37:29, na nilikwambia kwamba nitakuonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu ufufuo. Angalia maelezo haya.” Mwombe alete broshua yake, na mzungumzie fungu la 12-14 kwenye ukurasa wa 24 na 25 wa broshua hiyo. Muulize kama angependa kujifunza Biblia, au upange kuzungumzia fungu la 15 na 16 kwenye ziara itakayofuata.

Mapendekezo ya Kutoa—Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?

Baada ya kumsalimu mwenye nyumba, unaweza kusema:

“Matatizo na hali zenye kufadhaisha ni za kawaida katika maisha ya leo. Unafikiri maisha yalikusudiwa kuwa hivi? [Mruhusu ajibu.] Broshua hii inaonyesha kwamba kusudi la Mungu kuelekea wanadamu na dunia litatimizwa hatimaye. [Zungumzia picha iliyo kwenye ukurasa wa 20-21. Kisha usome fungu la 9 na ukazie Isaya 14:24 na 46:11.] Nitakaporudi, nitakuonyesha Maandiko yanayosema kwamba Mungu ataifanya dunia iwe Paradiso tena.” Mwachie broshua na upange kurudi.

Unaporudi, unaweza kusema:

“Wakati uliopita nilitaja kwamba Mungu anakusudia wanadamu waishi milele katika dunia paradiso. [Mwonyeshe tena picha iliyo kwenye ukurasa wa 20-21.] Ona kwamba Yesu, Petro, na Daudi walizungumza kuhusu Paradiso.” Fungua ukurasa wa 21-22, na uzungumzie fungu la 10-13. Muulize kama angependa kujifunza Biblia, au upange kuzungumzia mojawapo ya vichwa vidogo kwenye ukurasa wa 29-30.

**********

Mhubiri kijana anaweza kusema:

“Vijana wengi wa rika langu hawajui maisha yatakuwaje wakati ujao. Unafikiri maisha ya kizazi kinachokuja yatakuwa bora? [Mruhusu ajibu.] Biblia inasema kwamba wanadamu wote watakuwa na wakati ujao mzuri. [Mwonyeshe picha kwenye ukurasa wa 31, na usome maelezo ya picha. Kisha usome 2 Petro 3:13.] Broshua hii inazungumzia baraka ambazo Mungu atawaletea wanadamu. [Kazia vichwa vidogo vyenye herufi nzito kwenye ukurasa wa 29-30, na umtolee broshua hiyo.] Ningependa kurudi tena ili nikuonyeshe ahadi ya Mungu ya kukomesha vita vyote.” Panga kurudi.

Unaporudi, unaweza kusema:

“Nilipokutembelea tulizungumzia kwa ufupi kusudi la Mungu la kuifanya dunia kuwa paradiso tena. [Mwonyeshe tena picha kwenye ukurasa wa 31.] Ningependa kujua maoni yako kuhusu ahadi ya Mungu ya kukomesha vita vyote.” Mwombe alete broshua yake, kisha msome na kuzungumzia fungu la 3-6 kwenye ukurasa wa 29. Panga kuzungumzia fungu la 7 na 8 utakaporudi.

**********

Mtu mzima anapohubiri na mtoto, anaweza kujitambulisha pamoja na mtoto na kusema:

“Ukipenda, ________ anaweza kukuonyesha picha na kusoma andiko moja katika Biblia. [Mtoto amwonyesha picha na kusoma maelezo ya picha kwenye ukurasa wa 31, kisha asome Ufunuo 21:4.] Broshua hii inaeleza hatua ambayo Mungu atachukua kuelekea matatizo tunayokabili leo. [Kazia kwa ufupi vichwa vidogo vyenye herufi nzito kwenye ukurasa wa 29-30, na umtolee broshua.] Tutakaporudi, nitakuonyesha Biblia inasema nini kuhusu mwisho wa matatizo yote ya afya.”

Mtu mzima anaporudi, anaweza kusema:

“Tulipozungumza wakati uliopita, nilikwambia kwamba nitakuonyesha Biblia inasema nini kuhusu mwisho wa matatizo yote ya afya. Ona maelezo haya.” Mwombe alete broshua yake, kisha uzungumzie fungu la 9-14 kwenye ukurasa wa 29 wa broshua hiyo. Muulize kama angependa kujifunza Biblia, au upange kuzungumzia fungu la 15-17 utakaporudi.

Broshua kwa Ajili ya Watu wa Dini Zisizo za Kikristo

Lasting Peace and Happiness—How to Find Them

Unapomhubiria mwanafunzi Mchina unaweza kusema:

“Nimetambua kwamba wanafunzi wote hutaka amani na furaha. Unafikiri kwamba mambo hayo ni muhimu? [Mruhusu ajibu.] Je, hatutafurahia kuona maneno haya yaliyoandikwa zamani yakitimizwa?” Soma Zaburi 37:11, na umtolee broshua.—km 2/98 uku. 5.

“Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”

Unaweza kumwambia hivi mtu mwenye umri mkubwa aliye Mbudha:

“Huenda unahangaishwa kama ninavyohangaishwa na ongezeko kubwa la maoni yasiyofaa na jinsi yanavyowaathiri watoto wetu. Kwa nini kuna visa vingi vya ukosefu wa adili miongoni mwa vijana? [Mruhusu ajibu.] Je, unajua kwamba jambo hilo lilitabiriwa katika kitabu ambacho kilianza kuandikwa muda mrefu kabla ya kuanzishwa kwa dini ya Kiislamu, ya Kikristo, na ya Kihindu? [Soma 2 Timotheo 3:1-3.] Ona kwamba hali hizi zingekuwako licha ya elimu kuenea. [Soma mstari wa 7.] Kichapo hiki kilinisaidia kuelewa ukweli ambao wengi hawaujui. Je, ungependa kukisoma?”—km 8/99 uku. 8.

Why Should We Worship God in Love and Truth?

Utangulizi huu unaweza kumfaa Mhindu aliye na familia:

“Ninawatembelea watu wanaohangaishwa na hali ya maisha ya familia katika nchi nyingi leo. Unafikiri ni nini kinachoweza kudumisha umoja katika familia? [Mruhusu ajibu.] Watu fulani wanajua yale ambayo maandiko ya Wahindu yanasema kuhusu familia, lakini hawajawahi kulinganisha mambo hayo na yale ambayo Biblia inasema kuhusu suala hilo. Ningependa kukuonyesha jambo moja. [Soma Wakolosai 3:12-14.] Broshua hii inazungumzia maandishi matakatifu ya Wahindu na ya Biblia pia.” Mtolee broshua na umwonyeshe ukurasa wa 8-9 na 20-21.—km 9/99 uku. 8.

Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?

Unaweza kumwambia hivi kijana Mhindu:

“Bila shaka unamwamini Mungu. Unafikiri Mungu ana kusudi gani kutuhusu? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mwanzo 1:28.] Katika sehemu nyingi za ulimwengu, kuna idadi kubwa sana ya watu na pia kuna matatizo chungu nzima. Unafikiri Muumba yuko tayari kutusaidia kutatua matatizo yetu?” Mruhusu ajibu, kisha umtolee broshua.—km 9/99 uku. 8.

Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?

Unaweza kusema hivi unapomhubiria Myahudi:

“Wengi wetu wamehuzunishwa na kifo cha mpendwa. Unafikiri ni nini hutupata tunapokufa?” Mruhusu ajibu, kisha mwonyeshe sanduku “Kifo na Nafsi—Hizo Ni Nini?” katika ukurasa wa 22 wa broshua hiyo. Soma fungu la 17 katika ukurasa wa 23 kuhusu ufufuo. Taja kwamba Ayubu aliamini kwamba ufufuo utakuwako. Mtolee broshua, na upange kurudi ili mzungumzie maandiko yaliyo mwishoni mwa fungu la 17.—km-E 10/99 uku. 8.

Mwongozo wa Mungu —Njia Yetu ya Kwenda Paradiso

Unaweza kusema hivi unapomhubiria Mwislamu:

“Mimi huongea na Waislamu. Naelewa kwamba Waislamu wanamwamini Mungu mmoja tu na wanawaamini manabii wote. Je, ndivyo ilivyo? [Mruhusu ajibu.] Ningependa tuzungumzie unabii fulani wa zamani uliotabiri kwamba dunia itafanywa kuwa paradiso. Ninaweza kukusomea yale ambayo nabii huyu aliandika? [Mruhusu ajibu, kisha usome Isaya 11:6-9.] Unabii huu unafanya nifikirie maneno fulani katika Kurani ambayo yamo katika broshua hii.” Fungua ukurasa wa 9, na usome maneno yaliyoandikwa kwa herufi nzito. Akipendezwa, zungumzieni fungu la 7-9 katika ukurasa unaofuata.—km 11/99 uku. 8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki