-
“Utakuwa na Shangwe Kwelikweli”Mnara wa Mlinzi—2007 | Januari 1
-
-
Washiriki Zaidi wa Uzao wa Abrahamu
7. Sherehe ya Majuma ilikuwa nini?
7 Yesu ndiye Uzao ulioahidiwa huko Edeni na Yehova atamtumia ‘kuzivunja kazi za Ibilisi.’ (1 Yohana 3:8) Lakini, Yehova aliposema na Abrahamu, alionyesha kwamba “uzao” wa Abrahamu ungekuwa zaidi ya mtu mmoja tu. Ungekuwa “kama nyota za mbinguni na kama chembe za mchanga zilizo kando ya bahari.” (Mwanzo 22:17) Kutokea kwa washiriki wengine wa “uzao” huo kulionyeshwa kimbele na sherehe nyingine yenye shangwe. Siku 50 kuanzia Nisani 16, Waisraeli walisherehekea Sherehe ya Majuma. Sheria kuhusu sherehe hiyo inasema: “Mpaka siku inayofuata sabato ya 7 mtahesabu, siku 50, nanyi mtamtolea Yehova toleo jipya la nafaka. Kutoka katika makao yenu mtaleta mikate miwili iwe toleo la kutikisa. Itakuwa ya sehemu mbili za kumi za efa ya unga laini. Itaokwa ikiwa imetiwa chachu, kama matunda ya kwanza yaliyoiva kwa Yehova.”b—Mambo ya Walawi 23:16, 17, 20.
8. Ni jambo gani la maana lililotukia katika Pentekoste ya 33 W.K.?
8 Yesu alipokuwa duniani, Sherehe ya Majuma ilikuwa ikiitwa Pentekoste (kutokana na neno la Kigiriki linalomaanisha “-a 50”). Katika Pentekoste ya 33 W.K., Kuhani Mkuu zaidi, Yesu Kristo aliyefufuliwa, alimwaga roho takatifu juu ya kikundi kidogo cha wanafunzi 120 waliokusanyika Yerusalemu. Hivyo, wanafunzi hao wakawa wana wa Mungu waliotiwa mafuta na pia wakawa ndugu za Yesu Kristo. (Waroma 8:15-17) Wakawa pia taifa jipya, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Kuanzia hapo, taifa hilo dogo lingeongezeka na kuwa na washiriki 144,000.—Ufunuo 7:1-4.
9, 10. Kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta lilionyeshwa kimbele siku ya Pentekoste jinsi gani?
9 Kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta lilionyeshwa kimbele na ile mikate miwili iliyotiwa chachu ambayo ilitikiswa mbele za Yehova kila siku ya Pentekoste. Kutiwa chachu kwa mikate hiyo kulionyesha kwamba Wakristo watiwa-mafuta bado wangekuwa na chachu ya dhambi waliyorithi. Hata hivyo, wangeweza kumkaribia Yehova kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Yesu. (Waroma 5:1, 2) Kwa nini mikate miwili ilitumiwa? Huenda hilo lilionyesha uhakika wa kwamba wana hao wa Mungu waliotiwa mafuta wangetoka katika vikundi viwili, kwanza kutoka kwa Wayahudi wa asili, na baadaye kutoka kwa Watu wa Mataifa.—Wagalatia 3:26-29; Waefeso 2:13-18.
10 Mikate miwili iliyotolewa siku ya Pentekoste ilitokana na matunda ya kwanza ya mavuno ya ngano. Kwa njia inayolingana, Wakristo waliozaliwa kwa roho wanaitwa “sehemu fulani ya matunda ya kwanza ya viumbe vyake.” (Yakobo 1:18) Wao ndio wa kwanza kusamehewa dhambi kwa msingi wa damu iliyomwagwa ya Yesu, na hilo linawawezesha kupewa uhai usioweza kufa huko mbinguni ambako watatawala pamoja na Yesu katika Ufalme wake. (1 Wakorintho 15:53; Wafilipi 3:20, 21; Ufunuo 20:6) Wakiwa wana wa kimbingu, hivi karibuni ‘watachunga mataifa kwa fimbo ya chuma’ na kuona ‘Shetani akipondwa chini ya miguu yao.’ (Ufunuo 2:26, 27; Waroma 16:20) Mtume Yohana alisema: “Hao ndio wale wanaoendelea kumfuata Mwana-Kondoo popote anapoenda. Hao walinunuliwa kutoka kati ya wanadamu wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.”—Ufunuo 14:4.
-
-
“Utakuwa na Shangwe Kwelikweli”Mnara wa Mlinzi—2007 | Januari 1
-
-
b Wakati mikate miwili iliyotiwa chachu ilipotolewa kama toleo la kutikisa, mara nyingi kuhani aliibeba mikate hiyo kwenye viganja vyake, kisha akainua mikono yake na kuipeleka mikate hiyo huku na huku. Tendo hilo la kutikisa lilifananisha kutolewa kwa vitu vilivyotolewa dhabihu kwa Yehova.—Ona Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa wa 528 au Étude Perspicace des Écritures, Buku la 2, ukurasa wa 850, lililochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
-