-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
Wakati wa Mavuno Uliongojewa Sana
10, 11. (a) Kazi ya kuvuna inafanywa wakati gani? (b) Ngano ya mfano inakusanywa jinsi gani ndani ya ghala la Yehova?
10 Yesu anatuambia hivi: “Yale mavuno ni umalizio wa mfumo wa mambo, na wavunaji ni malaika.” (Mt. 13:39) Katika siku za mwisho za mfumo huu mwovu wa mambo, wana wa Ufalme wanakusanywa na kutenganishwa kutoka kwa watu wowote ambao ni kama magugu. Mtume Petro anatuambia hivi kuhusu jambo hilo: “Ni wakati uliowekwa wa hukumu kuanza na nyumba ya Mungu. Sasa ikiwa inaanza na sisi kwanza, basi mwisho wa wale wasioitii habari njema ya Mungu utakuwaje?”—1 Pet. 4:17.
11 Muda mfupi baada ya siku za mwisho au “umalizio wa mfumo wa mambo” kuanza, wale waliodai kuwa Wakristo wa kweli walianza kuhukumiwa ili kuamua ikiwa kwa kweli walikuwa “wana wa ufalme” au “wana wa yule mwovu.” “Kwanza” Babiloni Mkubwa alianguka, “ndipo” wana wa Ufalme wakakusanywa pamoja wakati kazi ya kuvuna ilipoanza. (Mt. 13:30) Lakini ngano ya mfano inakusanywa jinsi gani leo ndani ya depo au ghala la Yehova? Watu hao waliovunwa walijiunga na kutaniko la Kikristo ambalo limepangwa kitengenezo na ambalo linaendeleza ibada safi, ambamo wanakubaliwa na Mungu na kupata ulinzi wake, au walipata thawabu yao ya kwenda mbinguni.
12. Kazi ya kuvuna inaendelea kwa muda gani?
12 Hukumu inaendelea kwa muda gani? Yesu alisema kwamba kuna “majira” ya mavuno, kwa hiyo hukumu inaendelea kwa kipindi fulani. (Ufu. 14:15, 16) Hukumu ya watiwa-mafuta wakiwa mtu mmoja-mmoja inaendelea katika kipindi chote cha siku za mwisho. Itaendelea mpaka watiwe muhuri wa mwisho.—Ufu. 7:1-4.
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
“Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”
16, 17. Malaki alitoa unabii gani kuhusu hekalu la Mungu, na ulianza kutimizwa jinsi gani?
16 Watu ambao ni kama ngano “watang’aa kwa uangavu kama jua” wakati gani? (Mt. 13:43) Malaki alitabiri hivi kuhusu kusafishwa kwa hekalu la Mungu: “‘Kwa ghafula Bwana wa kweli atakuja kwenye hekalu Lake, ambaye ninyi mnamtafuta, na mjumbe wa agano mnayependezwa naye. Tazama! Atakuja hakika,’ asema Yehova wa majeshi. ‘Lakini ni nani atakayeistahimili siku ya kuja kwake, naye ni nani atakayesimama wakati atakapoonekana? Kwa maana atakuwa kama moto wa msafishaji na kama sabuni ya wafuaji wa nguo. Naye ataketi kama msafishaji na mtakasaji wa fedha naye atawatakasa wana wa Lawi; naye atawasafisha kama dhahabu na kama fedha, nao watakuwa kwa Yehova watu wanaotoa toleo la zawadi katika uadilifu.’”—Mal. 3:1-3.
17 Katika nyakati zetu, ni wazi kwamba unabii huo ulianza kutimizwa mwaka wa 1918 wakati Yehova, pamoja na “mjumbe wa agano,” Yesu Kristo, walipokagua hekalu la kiroho. Malaki anatuambia jambo linalotukia wakati kazi hiyo ya kusafisha inapokamilika: “Nanyi mtaona tena tofauti kati ya mwadilifu na mwovu, kati ya mtu anayemtumikia Mungu na mtu ambaye hajamtumikia.” (Mal. 3:18) Kuongezeka kwa utendaji wa Wakristo wa kweli waliotendeshwa tena kunaonyesha kwamba mavuno yalianza wakati huo.
18. Ni nini ambacho Danieli alitabiri kwamba kingetukia katika siku zetu?
18 Nabii Danieli alitabiri hivi kuhusu siku zetu: “Wale walio na ufahamu watang’aa kama mwangaza wa anga; na wale wanaoleta wengi kwenye uadilifu, watang’aa mpaka wakati usio na kipimo, milele kama nyota.” (Dan. 12:3) Ni nani hao wanaong’aa kwa uangavu sana? Si wengine ila ni Wakristo watiwa-mafuta, ngano ya kweli ambayo Yesu alitaja katika mfano wake kuhusu ngano na magugu! Umati mkubwa unaoongezeka wa kondoo wa mfano umetambua waziwazi ‘kukusanywa’ kwa Wakristo wa uwongo ambao ni kama magugu. Washiriki wa umati huo mkubwa ambao wanatazamia kuwa raia wa Ufalme wanashikamana na mabaki ya Waisraeli wa kiroho na wao pia wanaacha nuru yao iangaze katika ulimwengu wenye giza.—Zek. 8:23; Mt. 5:14-16; Flp. 2:15.
19, 20. “Wana wa ufalme” wanangoja nini kwa hamu, na tutazungumzia nini katika habari inayofuata?
19 Leo, “wana wa ufalme” wanangoja kwa hamu thawabu yao tukufu ya kimbingu. (Rom. 8:18, 19; 1 Kor. 15:53; Flp. 1:21-24) Hata hivyo, kabla ya wakati huo, ni lazima waendelee kuwa waaminifu, waendelee kuangaza kwa uangavu wakiwa tofauti kabisa na “wana wa yule mwovu.” (Mt. 13:38; Ufu. 2:10)
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
Mfano wa Ngano na Magugu
3. Mtu anayetajwa katika mfano huo anakabili tatizo gani na anaamua kulishughulikia jinsi gani?
3 Huu ndio mfano wa ngano na magugu: “Ufalme wa mbinguni umekuwa kama mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake. Watu wakiwa wamelala usingizi, adui yake alikuja na kupanda magugu katikati ya ngano, naye akaondoka. Wakati jani lilipoota na kuzaa matunda, magugu yalionekana pia. Kwa hiyo watumwa wa mwenye nyumba wakaja na kumwambia, ‘Bwana, je, hukupanda mbegu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje basi lina magugu?’ Akawaambia, ‘Adui, mtu fulani, alifanya hivyo.’ Wakamwambia, ‘Basi, je, unataka twende kuyakusanya?’ Akasema, ‘Hapana; ili, mnapoyakusanya magugu, msije mkang’oa ngano pamoja nayo. Acheni zikue pamoja mpaka wakati wa mavuno; na katika majira ya mavuno nitawaambia wavunaji, Kwanza kusanyeni magugu na kuyafunga matita-matita ili kuyateketeza motoni, ndipo nendeni mkusanye ngano ghalani mwangu.’”—Mt. 13:24-30.
4. (a) Mtu anayetajwa katika mfano huo ni nani? (b) Yesu alianza wakati gani na jinsi gani kupanda mbegu hiyo?
4 Mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake ni nani? Yesu anajibu swali hilo baadaye anapowaeleza hivi wanafunzi wake: “Mpandaji wa mbegu nzuri ni Mwana wa binadamu.” (Mt. 13:37) Yesu, ambaye ni “Mwana wa binadamu,” alitayarisha shamba katika kipindi cha miaka mitatu na nusu ya huduma yake duniani ili apande mbegu. (Mt. 8:20; 25:31; 26:64) Kisha kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K. na kuendelea, alianza kupanda mbegu nzuri, yaani, “wana wa ufalme.” Inaonekana kwamba mbegu hiyo ilipandwa wakati Yesu, akiwa mwakilishi wa Yehova, alipoanza kuwamwagia wanafunzi wake roho takatifu, na hivyo akawatia mafuta ili wawe wana wa Mungu.b (Mdo. 2:33) Mbegu hiyo nzuri ilikomaa na kuwa ngano. Kwa hiyo, Yesu alipanda mbegu nzuri ili mwishowe akusanye hesabu kamili ya wale ambao wangekuwa warithi na watawala wenzake katika Ufalme wake.
-