Kilimsukuma atende!
Mwanamume mmoja kutoka Caracas, jiji kuu la Venezuela, alimtembelea baba yake aliyezeeka, Rufino. Baba huyo aliishi La Loma, kijiji cha mbali mashambani. Mwana huyo alimpelekea Rufino kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.
Baadaye, Mashahidi wa Yehova kutoka Los Humocaros walikwenda kuhubiri La Loma. Walishangaa watu walipoendelea kusema kwamba Shahidi mmoja tayari alikuwa anawatembelea. Mashahidi hao walitatizika kwa sababu walijua kwamba hakukuwa na Mashahidi wanaoishi katika eneo hilo. Kisha mtu fulani alionyesha nyumba ya huyo mtu aliyedhaniwa kuwa ni Shahidi—ilikuwa nyumba ya Rufino!
Rufino alifurahi sana kukutana na wageni wake. Kwa nini watu katika kijiji chake walimtambua kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova? Naam, Rufino alikuwa ameanza kusoma kitabu Kuishi Milele, na alipofikia sura ya 13, aliona picha za Yesu akiwatuma wafuasi wake katika kazi ya kuhubiri. Rufino alifikia mkataa kwamba leo Wakristo lazima wafanye kazi hiyo. Hivyo alianza kushiriki pamoja na jirani zake kweli za Biblia ambazo alikuwa anajifunza.
Funzo la kawaida la Biblia lilianzishwa na Rufino, na aliambiwa kuhusu mikutano ya kutaniko. Jumapili iliyofuata alikuwa katika Jumba la Ufalme. Ingawa Rufino alikuwa na umri wa miaka 80, alitembea kwa miguu kwa muda wa saa tatu ili kufika hapo! Kuanzia siku hiyo na kuendelea, kamwe hakukosa mkutano isipokuwa alipokuwa mgonjwa sana. Hata alijiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na alitoa hotuba nzuri. Mwaka uliopita Rufino alikuwa mgonjwa, na alikufa katika Julai 1996 akiwa na tumaini imara la ufufuo katika dunia paradiso.
Twaamini kwamba wewe pia utafaidika kwa kusoma kitabu chenye kurasa 256 chenye picha nzuri, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Ikiwa ungependa kupokea nakala ya kitabu hicho au ungependa kuwa na funzo la Biblia la nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A, Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ihusuyo katika ukurasa 5.