-
Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Estonia
Helgi, mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 ambaye hakuwa akiishi na wazazi wake waliotalikiana, alipendezwa na kweli na akaanza kujifunza Biblia. Mwanzoni hakuhudhuria mikutano mingi kwa sababu alikuwa akitumia wakati wake mwingi akiimba katika bendi fulani. Alipozidi kuthamini kweli, alianza kufanya mabadiliko maishani. Aliwaeleza washiriki wengine wa bendi yao kwa nini hangeweza kuwatumbuiza watu siku za mikutano. Alijiandikisha kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na akafanya maendeleo na kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa. Alishiriki katika mashindano ya kitaifa ya uimbaji ambapo mshindi angepewa mkataba na kampuni maarufu ya kurekodi. Ingawa wasanii wengi walikataliwa katika majaribio ya kwanza, Helgi alipendwa na waamuzi na akasonga hadi kwenye hatua iliyofuata ya mashindano hayo. Hata hivyo, mashindano yaliyofuata yangefanywa wakati ambapo alipaswa kutoa hotuba yake ya kwanza kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Angefanya nini? Mama yake ambaye si Shahidi wa Yehova alipendekeza kwamba akose kuitoa hotuba yake au aiahirishe. Helgi alisema kwamba suala halikuwa kutoa hotuba tu bali lilikuwa kuhusu kile alichotanguliza maishani, mambo ya kiroho au ya kimwili. Alifikiria jambo hilo kwa uzito na akaamua kutoa hotuba yake badala ya kwenda kwenye mashindano ya uimbaji. Helgi alitoa hotuba hiyo na mama yake akaheshimu uamuzi wake.
Baadaye ripota mmoja wa televisheni alihudhuria Kusanyiko la Wilaya la “Mfuateni Kristo!” ili kuripoti kuhusu kusanyiko hilo na ubatizo. Alipomwona Helgi akiingia kwenye kidimbwi cha ubatizo, alichukua video ya ubatizo wake na baadaye akamhoji. Jioni hiyo, ripoti hiyo ilikuwa katika habari na ilitia ndani video yake akishiriki kwenye hatua ya mapema ya mashindano ya uimbaji na ikamalizia kwa ubatizo wake huku akisema hivi kwa tabasamu changamfu, “Huu ndio uamuzi bora zaidi nimewahi kufanya.”
-
-
Kuhuburi na Kufundisha Ulimwenguni Pote2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 58]
Helgi (kulia) akitoa hotuba katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-