-
Zidi Kufanya Maendeleo ya Kiroho!Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
Mfikirie Anthony, aliyebatizwa akiwa mchanga. “Nilikuwa mtoto wa kwanza katika familia yetu kubatizwa,” yeye asimulia. “Baada ya kubatizwa, nilikumbatiwa kwa shauku na mama yangu. Sikuwa nimewahi kumwona akiwa mwenye furaha hivyo. Kulikuwa na shangwe nyingi kwelikweli, nami nilijihisi mwenye nguvu sana.” Hata hivyo, kulikuwepo na sababu nyingine ya kuwepo na shangwe nyingi hivyo. “Kwa muda mrefu, hakukuwa vijana wowote waliobatizwa katika kutaniko letu,” Anthony aendelea. “Kwa hiyo nilijivuna sana. Pia nilijivunia maelezo yangu na hotuba zangu mikutanoni. Kusifiwa na kukubaliwa na watu kukawa jambo la maana zaidi kuliko kumletea Yehova sifa. Kwa kweli sikuwa na uhusiano wa karibu naye.”
Sawa na Anthony, huenda watu fulani wakawa wamejiweka wakfu, wakitaka kuwapendeza watu wengine badala ya kutaka kumpendeza Yehova. Ingawa hivyo, Mungu huwatarajia watu hao watimize ahadi yao ya kumtumikia. (Linganisha Mhubiri 5:4.) Mara nyingi ni vigumu kwao kufanya hivyo ikiwa hawampendi Mungu kibinafsi. Anthony akumbuka: “Ile shangwe kubwa niliyokuwa nayo nilipobatizwa ilikuwa ya punde tu. Mwaka mmoja haukupita kabla sijafanya kosa zito na kukaripiwa na wazee wa kutaniko. Kurudia-rudia mwenendo mbaya kulinifanya nitengwe na ushirika wa kutaniko. Miaka sita baada ya kujiweka wakfu kwa Yehova, nilikamatwa na kufungwa kwa sababu ya kuua kimakusudi.”
-
-
Zidi Kufanya Maendeleo ya Kiroho!Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
Namna gani Anthony? “Nilianza kufikiria wakati nilipokuwa na miradi mingi kwelikweli ya kiroho iliyohusisha kufanya mapenzi ya Yehova,” yeye akumbuka. “Hilo liliumiza. Lakini kupitia maumivu hayo yote na kutamaushwa, niliukumbuka upendo wa Yehova. Ilichukua muda fulani kabla sijaweza kusali kwa Yehova, lakini nilisali, nikamfunulia moyo wangu wote, na kumwomba msamaha. Pia nilianza kujifunza Biblia nami nilishangaa kujua kadiri nilivyokuwa nimeisahau na jinsi kwa kweli nilijua machache sana juu ya Yehova.” Ingawa bado Anthony hajamaliza kifungo chake kwa sababu ya uhalifu wake, yeye husaidiwa na Mashahidi wenyeji naye anaelekea kupona kiroho. Kwa shukrani, Anthony asema hivi: “Kwa sababu ya Yehova na tengenezo lake, nimeweza kuuvua utu wa hapo zamani, nami najitahidi kuuvaa utu mpya kila siku. Uhusiano wangu na Yehova ni wa maana zaidi kwangu sasa.”
-