-
Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye KudumuHuduma ya Ufalme—1997 | Machi
-
-
2 Mlangoni na hata barabarani, unaweza kujaribu kutumia trakti “Furahia Maisha ya Familia” kuanzisha mazungumzo. Unaweza kuuliza:
◼ “Kukiwa na mahangaiko yote ambayo maisha ya kisasa hutuletea, je, wafikiri inawezekana kuwa na maisha ya familia yenye furaha kweli? [Ruhusu itikio.] Trakti hii hutuhakikishia kwamba inawezekana. Je, ungependa kuisoma?” Ikikubaliwa, unaweza kuendelea kusema: “Kwa kuwa unapendezwa na jambo hili, labda pia utafurahia kitabu hiki ambacho huandaa ushauri wenye kina wa jinsi ya kupata furaha katika familia.” Onyesha yaliyomo katika kitabu Furaha ya Familia. Onyesha vichwa vya sura vichache vyenye kuvutia. Fungua ukurasa wa 10, na usome kuanzia sentensi ya mwisho ya fungu la 17 hadi mwisho wa fungu la 18. Toa kitabu. Eleza kwamba una mengi ya kushiriki, na uulize ni lini unapoweza kurudi tena.
-
-
Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye KudumuHuduma ya Ufalme—1997 | Machi
-
-
4 Unapoongea na wanadarasa wenzako shuleni au vijana katika eneo, huenda ukapata itikio kwa swali hili:
◼ “Ni jambo la maana kadiri gani kwa wazazi na watoto wao kudumisha mawasiliano? [Ruhusu itikio.] Ona jinsi kitabu hiki kuhusu maisha ya familia kinavyosema juu ya somo la ‘Uwasiliano wa Haki na Ulio Wazi.’ [Soma fungu la 4 lote, ukikazia andiko la Mithali 15:22, na sentensi ya kwanza ya fungu la 5 kwenye ukurasa wa 65 katika kitabu Furaha ya Familia.] Mafungu yanayofuata yanaandaa madokezo yenye kutumika ya jinsi ya kuboresha mawasiliano katika familia. Kitabu hiki kina kichwa Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Eleza kwamba utarudi baadaye ujue maelezo yake juu ya yale anayosoma.
-
-
Kusaidia Familia Zipate Wakati Ujao Wenye KudumuHuduma ya Ufalme—1997 | Machi
-
-
6 Ukimkuta mzazi katika mahubiri ya nyumba hadi nyumba, au labda kwenye bustani au mahali pa kuchezea, unaweza kuamsha kupendezwa kwa kusema:
◼ “Nina hakika utakubali kwamba kulea watoto leo ni jambo gumu sana. Unafikiri ni nini kiwezacho kulinda watoto wako na mavutano yasiyofaa? [Ruhusu itikio.] Hapa pana ushauri bora kabisa ambao nimethamini.” Simulia kielezi katika fungu la 1, na usome fungu la 2 kwenye ukurasa wa 90 katika kitabu Furaha ya Familia. Eleza jinsi kinavyotoa mwelekezo wenye matokeo kulinda familia na mavutano yenye kuharibu. Acha kitabu, na uwe tayari kujibu swali lolote linalotokea.
-