Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kushiriki na Wengine Siri ya Kupata Furaha ya Familia
    Huduma ya Ufalme—1997 | Septemba
    • 2 Ungeweza kuanza kwa kutokeza swali kama vile:

      ◼ “Je, umetambua kwamba familia nyingi zinaona kuwa jambo gumu kuvumilia mikazo ya maisha? [Ruhusu itikio.] Ripoti zaonyesha kwamba watu wengi huona magumu nyumbani. Unaamini ni nini kingezisaidia familia zipate uthabiti na furaha nyingi zaidi? [Ruhusu itikio.] Kwa kuwa Mungu alianzisha mpango wa familia, je, halingekuwa jambo la busara kuchunguza miongozo ambayo ametoa? [Soma 2 Timotheo 3:16, 17.] Maagizo hayo yenye manufaa yanaonyeshwa katika kitabu hiki, Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Kisha umwulize mtu huyo lile analohisi ni tatizo la kawaida la familia, onyesha sura ambayo inazungumzia tatizo hilo, toa kitabu.

  • Kushiriki na Wengine Siri ya Kupata Furaha ya Familia
    Huduma ya Ufalme—1997 | Septemba
    • 4 Njia nyingine ya kuanzisha mazungumzo ni kutaja tatizo moja, labda kwa kusema:

      ◼ “Ijapokuwa kila mtu anataka kuhisi uradhi na kutosheka, yaonekana familia nyingi kwa kweli hazijafaulu katika jambo hili. Unafikiri ni nini kingewasaidia wapate furaha ya kweli? [Ruhusu itikio.] Zamani za kale, Biblia ilionyesha aina ya matatizo ambayo tungeona katika familia leo. [Soma 2 Timotheo 3:1-3.] Hata hivyo, Biblia pia huambia familia jambo la kufanya ili kutatua matatizo hayo na kupata furaha yenye kudumu. Kanuni zake zimeonyeshwa katika kitabu hiki, Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Kisha uonyeshe sanduku la kupitia mwishoni mwa sura ihusuyo, soma, na utoe kitabu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki