Kwa Nini Hakuamini Katika Mungu?
OLESYA, mwanamke kijana katika Rustavi, Georgia, ambayo hapo zamani ilikuwa jamhuri katika Muungano wa Sovieti, aliwaonyesha wageni wawili picha ya wazazi wake na kusema kwa mshangao: “Ikiwa kulikuwa na Mungu, hangeruhusu wazazi wangu wafe walipokuwa na umri mchanga namna hiyo!” Baada ya mume wa Olesya, Tamazi, kufika nyumbani, wageni hao waliwaachia broshua Furahia Milele Maisha Duniani! na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.”
Ziara ya kurudia ilipofanywa kwa wenzi hao, Olesya alikuwa amesoma broshua “Tazama!” na alitaka kujifunza Biblia. Alipendezwa na aliyosoma. Wakati wa mazungumzo yaliyofuata, alifanya upesi kufungua ile broshua na kusoma sehemu alizokuwa ametia alama. Alivutiwa na hoja zake nzuri.
Kwa kielelezo, broshua hiyo husema: “Yale maajabu yenye utukufu yanayotuzunguka—maua, ndege, na wanyama, uumbaji wa ajabu unaoitwa wanadamu, ile miujiza ya uhai na uzawa—yote hayo yanashuhudia kwamba kuna Mtaalamu Mwenye Akili asiyeonekana aliyeyafanyiza. (Warumi 1:20) Palipo na fikira, pana akili. Palipo na akili, pana mtu. Fikira kuu ni ile ya Mtu Mkuu, Muumba wa vitu vyote vilivyo hai, aliye Chemchemi yenyewe ya uhai. (Zaburi 36:9) Ndiyo, Muumba anastahili sifa na ibada yote.—Zaburi 104:24; Ufunuo 4:11.”
Baadaye Olesya alisema kwa faragha kwamba ahadi ya Mungu ya kufufua wapendwa waliokufa ndiyo iliyomchochea kujifunza Biblia. Twaamini kwamba wewe pia utanufaika kutokana na habari yenye kuimarisha imani iliyo ndani ya broshua hizi. Ikiwa wataka nakala ya Furahia Milele Maisha Duniani! na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” au ungependa mtu fulani akutembelee nyumbani mwako ili kuongoza funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.