Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakristo Wote wa Kweli Ni Waeneza-evanjeli
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Januari 1
    • Kichapo Catholic World Report chasema: ‘Kwa sababu ya malalamiko mengi ya Kanisa la Othodoksi, kugeuza watu imani kumeanza kuonwa kama jambo linalofanywa kwa nguvu.’

      13. Ni mifano gani inayoonyesha kugeuza watu imani ambako ni hatari?

      13 Je, ni hatari kugeuza watu imani? Ndiyo. Yesu alisema kwamba kugeuza watu imani kulikofanywa na waandishi na Mafarisayo kulikuwa hatari kwa wageuzwa-imani. (Mathayo 23:15) Bila shaka ni kosa ‘kugeuza watu imani kwa nguvu.’ Kwa mfano, kulingana na mwanahistoria Yosefu, wakati Mmakabayo John Hyrcanus alipowatiisha Waidumea, “aliwaruhusu wabaki katika nchi yao maadamu wangetahiriwa na wangekuwa tayari kutii sheria za Wayahudi.” Ikiwa Waidumea wangeishi chini ya utawala wa Wayahudi, wangelazimika kufuata dini ya Wayahudi. Wanahistoria wanatuambia kwamba katika karne ya nane W.K., Charlemagne aliwashinda wapagani wa Saxon wa kaskazini mwa Ulaya na kuwalazimisha kikatili wageuze imani yao.a Hata hivyo, je, kweli Waidumea au watu wa Saxon walikuwa wamegeuza imani yao kwa unyofu? Kwa mfano, je, Mfalme Herode wa Idumea alikuwa mwaminifu kwa Sheria ya Musa iliyopuliziwa wakati alipojaribu kuua kitoto Yesu?—Mathayo 2:1-18.

      14. Baadhi ya mishonari wa Jumuiya ya Wakristo hulazimishaje watu wageuze imani yao?

      14 Je, watu hulazimishwa kugeuza imani leo? Wengine hulazimishwa kufanya hivyo. Imeripotiwa kwamba mishonari fulani wa Jumuiya ya Wakristo hutoa msaada wa masomo kwa wageuzwa-imani wakasomee ng’ambo. Au huenda wakamlazimisha mkimbizi mwenye njaa asikilize mahubiri yao ndiposa wampe chakula. Kulingana na taarifa iliyotolewa katika mwaka wa 1992 kwenye kusanyiko la makasisi wa Kanisa la Othodoksi, “mara nyingine watu hugeuzwa imani kwa kushawishiwa kwamba watapewa vitu vya kimwili na nyakati nyingine kwa kutumia nguvu.”

      15. Je, Mashahidi wa Yehova hugeuza watu imani kama wengine wafanyavyo siku hizi? Eleza.

      15 Ni kosa kulazimisha watu wabadili dini. Bila shaka, Mashahidi wa Yehova hawafanyi hivyo.b Kwa hiyo, hawageuzi watu imani kama wengine wafanyavyo siku hizi. Badala yake, kama Wakristo wa karne ya kwanza, wao huhubiria kila mtu habari njema. Mtu yeyote anayekubali habari njema kwa kupenda, hutiwa moyo atwae ujuzi zaidi kwa kujifunza Biblia. Watu hao wenye kupendezwa hujifunza kuwa na imani inayotegemea kabisa ujuzi sahihi wa Biblia kuhusu Mungu na makusudi yake. Hivyo, wanaliitia jina la Mungu, Yehova, ili kupata wokovu. (Waroma 10:13, 14, 17) Ni juu yao kuamua kama watakubali au watakataa habari njema. Hawalazimishwi. Kama watu wangelazimishwa, kugeuza watu imani hakungekuwa na maana yoyote. Ili mtu akubaliwe na Mungu, lazima ibada yake itoke moyoni.—Kumbukumbu la Torati 6:4, 5; 10:12.

  • Wakristo Wote wa Kweli Ni Waeneza-evanjeli
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Januari 1
    • a Kulingana na The Catholic Encyclopedia, wakati wa Marekebisho Makuu ya Kidini, kulazimisha watu wakubali dini fulani kulionyeshwa na wito huu wa Kilatini: Cuius regio, illius et religio (Kwa msingi, wito huo wamaanisha: “Yeyote yule anayetawala nchi ndiye anayeamua dini itakayofuatwa.”)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki