Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kufikia mwaka wa 1992, kikundi kilichokutana kwa ajili ya Funzo la Kitabu la Kutaniko na Funzo la Mnara wa Mlinzi katika mji wa Herceg Novi kiliongezeka na kuwa na watu 15.” Savo, pamoja na mke wake na binti, waliendelea kufanya maendeleo wakabatizwa mwaka wa 1993. Leo kuna Jumba la Ufalme lenye wahubiri 25 katika mji huo wa pwani wenye kuvutia sana.

      Mwanzoni mwa miaka ya 1990, kikundi cha wahubiri kilikutana katika mji mkuu wa Podgorica. Kikundi hicho kiliendelea kukua, na katika mwaka wa 1997 mipango ilifanywa ya kununua uwanja wa kujenga Jumba la Ufalme. Uwanja ambao ndugu walinunua ulizungukwa na ukuta, na hivyo ndugu wakaamua kutoubomoa ili wawe na faragha. Lakini ofisa wa polisi aliyeishi katika chumba cha chini katika jengo jirani aliwaomba wabomoe ukuta huo ili mwangaza ufike kwenye chumba chake chenye giza. Ili wawe na uhusiano mzuri na jirani huyo, akina ndugu walikubali kuubomoa ukuta huo na kuweka ua. Walibarikiwa sana kwa sababu ya kumwonyesha jirani yao upendo!

      Wapangaji wengine wa jengo hilo walipoanza kuwasumbua akina ndugu, ofisa huyo wa polisi aliwaonya kwamba angehakikisha wameshtakiwa ikiwa wangevamia Jumba la Ufalme. Sasa akina ndugu wana Jumba zuri sana la Ufalme, vilevile nyumba ya mapainia wa pekee, na kibanda kikubwa cha kuegesha magari ambacho kinaweza pia kutumiwa kwa ajili ya makusanyiko.

      Hata hivyo, akina ndugu katika mji wa Nikšić walipata matatizo. Walinunua uwanja mwaka wa 1996, lakini majirani wao walikataa kabisa Jumba la Ufalme lisijengwe. Ndugu walilinda jengo hilo usiku na mchana, wakiogopa kwamba majirani wao wangejaribu kuliharibu. Siku moja, kasisi wa eneo hilo alikusanya umati wa watu 200, wakavamia jengo hilo wakiwa wamebeba bunduki na fimbo. Walifyatua risasi hewani na kuanza kubomoa Jumba la Ufalme, jiwe kwa jiwe. Polisi walisimama kando tu bila kuchukua hatua yoyote.

      Ndugu waliposhindwa kusuluhisha tatizo hilo kwa amani, walitafuta jengo lingine. Miaka minne baadaye, walipata jengo lingine, wakalirekebisha na kulifanya kuwa Jumba la Ufalme. Mwanzoni, ilionekana kwamba majirani hawakuwa na tatizo, lakini baada ya miezi michache, Jumba hilo la Ufalme liliteketezwa na watu wasiojulikana. Hata hivyo, ndugu zetu waliazimia kuendelea na hawakukata tamaa. Walijitahidi sana wakajenga upya jumba hilo. Tangu wakati huo hawajasumbuliwa tena.

  • Nchi Ambazo Zilikuwa Sehemu ya Yugoslavia
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 243]

      Kuhubiri huko Podgorica; Jumba la Ufalme huko Podgorica

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki