-
“Mimi Niko Tayari Kwenda”Mnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2016 | Na. 3
-
-
Ona kwamba Rebeka hakujitolea tu kuwapa ngamia kumi maji kidogo ya kunywa, bali alitaka kuwapa maji mengi hadi watakapotosheka. Ngamia mmoja mwenye kiu sana anaweza kunywa zaidi ya lita 95 za maji! Ikiwa ngamia wote kumi walikuwa na kiu sana, basi Rebeka alifanya kazi hiyo ngumu kwa saa nyingi. Hata hivyo, inaonekana ngamia hao hawakuwa na kiu sana.a Je, Rebeka alijua jambo hilo alipojitolea kuwapa maji? Hapana. Alikuwa tayari, hata alikuwa na hamu ya kufanya kazi kwa bidii sana ili kumwonyesha ukarimu mzee huyo mgeni. Mwanamume huyo alikubali msaada wake. Kisha alimtazama kwa makini kila mara alipokuwa akifanya kazi ya kwenda na kurudi ili kujaza mtungi wake na kumimina maji katika chombo cha kunyweshea wanyama.—Mwanzo 24:20, 21.
Rebeka alikuwa mwenye bidii na mkarimu
-
-
“Mimi Niko Tayari Kwenda”Mnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2016 | Na. 3
-
-
Inaonekana Rebeka aligundua kuwa mzee huyo alikuwa akimtazama. Si kwamba Rebeka alionekana kwa njia isiyofaa bali mwanaume huyo alikuwa akistaajabu na kufurahia bidii yake. Rebeka alipomaliza kazi, mwanamume huyo alimpa zawadi, yaani, vito vyenye thamani! Kisha akamuuliza: “Wewe ni binti ya nani? Tafadhali niambie. Je, mna nafasi yoyote nyumbani kwa baba yako tukae usiku huu?” Mwanaume huyo alifurahi sana alipoelezwa kuhusu familia yao. Labda akiwa amesisimka sana, Rebeka akajibu hivi: “Tuna majani na chakula kingi cha mifugo, pia mahali pa kukaa usiku,” hilo lilikuwa jambo zuri kwa kuwa mwanaume huyo mzee alikuwa na watu wengine aliosafiri nao. Kisha Rebeka akatangulia nyumbani ili kumwambia mama yake kilichotokea.—Mwanzo 24:22-28, 32.
-