-
Faraja kwa WanaotesekaMnara wa Mlinzi—2003 | Januari 1
-
-
Mungu hakuwaumba wanadamu wateseke. Badala yake, aliwapa wanadamu wawili wa kwanza, Adamu na Hawa, akili na miili mikamilifu, akawatayarishia shamba lenye kupendeza liwe makao yao, na akawapa kazi muhimu na yenye kuridhisha. (Mwanzo 1:27, 28, 31; 2:8) Hata hivyo, wangeendelea kuwa wenye furaha tu iwapo wangetambua utawala wa Mungu na kwamba ana haki ya kuamua yaliyo mema na yaliyo mabaya. Amri hiyo ya Mungu iliwakilishwa na mti ulioitwa “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.” (Mwanzo 2:17) Adamu na Hawa wangeonyesha ujitiisho wao kwa Mungu kama wangalitii amri yake ya kutokula matunda ya mti huo.a
-
-
Faraja kwa WanaotesekaMnara wa Mlinzi—2003 | Januari 1
-
-
a Kielezi-chini kwenye Mwanzo 2:17 katika tafsiri ya The Jerusalem Bible kinaeleza “ujuzi wa mema na mabaya” kuwa “uwezo wa kuamua . . . yaliyo mema na yaliyo mabaya kisha kutenda kulingana na uamuzi huo, yaani, dai la kuwa huru kabisa kujiamulia yaliyo mema na yaliyo mabaya na hivyo kukataa kutambua kwamba uliumbwa.” Kinaongeza kusema: “Dhambi ya kwanza ilikuwa ni shambulio dhidi ya haki ya Mungu ya kutawala.”
-