-
Kupata Shangwe ya Uhusiano Mchangamfu Kati ya WakweAmkeni!—1990 | Desemba 8
-
-
Kukitambua Kifungo Kipya
Biblia hutoa picha yenye kueleweka wazi juu ya mpango wa ndoa ya Kimaandiko. Baada ya Mungu kuumba wanadamu wawili wa kwanza na kuwaleta pamoja, alianzisha kanuni inayofuata. “Mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.” (Mwanzo 2:24) Kwa hiyo ni lazima mume na mke hao waliofunga ndoa karibuni watambue kwamba wameingia katika kifungo kipya. Ni lazima sasa washikamane wakiwa kiungo kimoja chenye kujitegemea hata ingawa huenda wakaishi pamoja na wakwe zao.
Hata hivyo, kuacha baba na mama hakumaanishi kwamba watoto wafungapo ndoa waweza kugeuzia wazazi wao kisogo na kwamba hawahitaji tena kuwastahi na kuwaheshimu. “Usimdharau mama yako akiwa mzee,” Biblia yaonya kwa upole. (Mithali 23:22) Hata hivyo, ndoa ifanywapo, huwa kuna rekebisho katika mahusiano. Maadamu kila mshiriki wa familia akumbuka hilo vizuri, hao mume na mke vijana waweza kunufaika na ujuzi na hekima ya wazazi.
-
-
Kupata Shangwe ya Uhusiano Mchangamfu Kati ya WakweAmkeni!—1990 | Desemba 8
-
-
Basi, mume awezaje kushiriki kwa bidii katika kuleta amani katika familia yake? Mitsuharu asema kwamba utumizi wake wa kanuni za Biblia ulisaidia familia yake. “Kifungo kilicho kati ya mama na mwana wake ni imara sana hata ingawa mwana amekua akawa mtu mzima,” yeye akiri, “hivyo basi ni lazima mwana afanye jitihada yenye ufahamu ili ‘amwache baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe.’” Yeye alitumia kanuni hiyo kwa kuzungumza pamoja na mke wake tu mambo yanayohusu kutunza watoto na kuwalea, naye hakulinganisha mke wake na mama yake katika kazi za nyumbani. “Sasa,” yeye aendelea kusema, “sisi na wazazi wangu hustahiana. Kila mmoja wetu ajua ni wapi uchukivu utatokea kwa kuingilia mambo na ni wapi msaada na ushirikiano utathaminiwa.”
Kwa kuongezea ‘kuambatana na mkewe,’ ni lazima mume awe mpatanishi kati ya mama yake na mke wake. (Mwanzo 2:24) Yeye ahitaji kuwa msikilizaji mwema na kuwaacha wamimine mioyo yao. (Mithali 20:5) Mume mmoja, ambaye amejifunza kushughulikia hali kwa busara, kwanza hutafuta kujua hisia za mke wake. Halafu yeye huongea na mama yake juu ya masuala yahusikayo, mke wake akiwapo. Kwa kujitwalia sehemu yake hivyo akiwa mfanya amani, mwana aweza kusaidia kufanyiza mahusiano yenye kupendeza nyumbani kati ya wanawake hao wawili awapendao.
-