-
Namna ya Kuimarisha Vifungo vya NdoaMnara wa Mlinzi—1993 | Agosti 15
-
-
Hata hivyo, Yesu hakuwa akipendekeza kwamba watu wataliki wenzi wasio waaminifu. Ni uamuzi wa mwenzi asiye na hatia kupima matokeo yanayohusika na kuamua kama yeye ataka talaka. Wake wanaofikiria talaka kwa msingi huo wa Kimaandiko huenda pia wakataka kufikiria taarifa ya Mungu alipomhukumu mwanamke wa kwanza kwa ajili ya dhambi yake. Kuongezea hukumu ya kifo, Mungu alimwambia Hawa kimahususi: “Tamaa yako [uchu wako, New World Translation] itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.” (Mwanzo 3:16) Commentary on the Old Testament, ya C. F. Keil na F. Delitzsch, inaeleza “uchu” huo kuwa “tamaa iliyo kama ugonjwa.” Kwa kweli, uchu huo si wenye nguvu hivyo katika kila mke, lakini mke asiye na hatia anapofikiria talaka, angekuwa na hekima kufikiria mahitaji ya hisia za moyoni ambayo wanawake wamerithi kutoka kwa Hawa. Hata hivyo, kwa kuwa ngono ya nje ya ndoa kwa upande wa mwenzi mwenye hatia ingeweza kumsababisha mwenzi asiye na hatia aambukizwe magonjwa ya kupitishwa kingono, kutia na UKIMWI, wengine wameamua kutaliki kama vile Yesu alivyoeleza.
-
-
Namna ya Kuimarisha Vifungo vya NdoaMnara wa Mlinzi—1993 | Agosti 15
-
-
Hukumu ya Yehova juu ya Adamu na Hawa ilitabiri chanzo kingine zaidi cha matatizo ambayo yangetokea. Kuhusu uhusiano wake na mume wake, Yehova alimwambia Hawa hivi: “Atakutawala.” Waume wengi leo, kama vile Isao aliyetajwa katika makala yetu ya kwanza, wanawatawala wake zao katika njia isiyo na huruma bila kufikiria hisia za wake zao. Lakini, wake wengi wanaendelea kuwa na uchu wa kuvuta fikira za waume zao. Uchu huo usiporidhishwa, huenda wake wakadai ufikirio huo kwa lazima na kutenda kwa ubinafsi. Kwa kuwa waume wengi ni wenye kutawala na wake wengi wana uchu wa kuvuta fikira za waume zao, ubinafsi huenea, na amani kutoweka. Katika ripoti moja yenye kichwa “Namna ya Kuchanganua Talaka za Leo,” Shunsuke Serizawa alisema hivi: “Tukipuuza tatizo la msingi linalohusu suala hili, yaani, kwamba watu wana mwelekeo wa kutanguliza mapendezi yao wenyewe, kwa ghafula ingekuwa haiwezekani tena kuchanganua talaka leo.”
-