YEHOVA-YIRE
(Yehova-yire) [Yehova Atahakikisha [Jambo] Hilo; Yehova Ataandaa].
Ni eneo lililo kwenye mojawapo ya milima ya nchi ya Moria ambapo Abrahamu aliona kondoo-dume akiwa amenaswa kichakani, basi akamtoa dhabihu badala ya kumtoa Isaka. Abrahamu aliamini kwamba kondoo-dume huyo ameandaliwa na Yehova, kwa hiyo, akaliita eneo hilo Yehova-yire. Mapokeo ya zamani yanasema kwamba hekalu la Sulemani lilijengwa kwenye eneo hilo.—Mwa 22:2, 13, 14; tazama MORIA.