Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Ni Nani Ameijua Akili ya Yehova?”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • 13. Kuelewa njia ya Yesu ya kufikiri kunatusaidia jinsi gani?

      13 Kuelewa njia ya Yesu ya kufikiri kunaweza kutusaidia kuelewa masimulizi ya Maandiko ambayo huenda ni vigumu kuyaelewa. Kwa mfano, fikiria maneno ambayo Yehova alimwambia Musa baada ya Waisraeli kutengeneza ndama wa dhahabu wa kuabudu. Mungu alisema hivi: “Nimewatazama watu hawa na, kumbe, ni watu wenye shingo ngumu. Basi sasa, niache, ili hasira yangu iwake juu yao nami niwaangamize, nami nikufanye wewe kuwa taifa kubwa.”—Kut. 32:9, 10.

      14. Musa alitenda jinsi gani baada ya kusikia maneno ya Yehova?

      14 Simulizi hilo linaendelea kusema hivi: “Musa akaanza kuutuliza uso wa Yehova Mungu wake na kusema: ‘Kwa nini, Ee Yehova, hasira yako iwake juu ya watu wako ambao uliwatoa katika nchi ya Misri kwa nguvu kuu na kwa mkono wenye nguvu? Kwa nini Wamisri waseme, “Aliwatoa kwa nia mbaya ili awaue katikati ya milima na kuwaangamiza kutoka katika uso wa nchi”? Geukia mbali uiache hasira yako inayowaka na ujute kuhusu uovu huo juu ya watu wako. Wakumbuke Abrahamu, Isaka na Israeli watumishi wako, uliowaapia kwa jina lako mwenyewe, kwa kuwa uliwaambia, “nitauzidisha uzao wenu kama nyota za mbinguni, nayo nchi hii yote ambayo nimeichagua, nitaupa uzao wenu, ili kwa kweli wapate kuimiliki mpaka wakati usio na kipimo.”’ Naye Yehova akaanza kujuta juu ya ule uovu aliokuwa amesema kwamba atawafanyia watu wake.”—Kut. 32:11-14.a

      15, 16. (a) Ni nafasi gani ambayo Musa alipata kwa sababu ya maneno ambayo Yehova alisema? (b) Yehova ‘alianza kujuta’ katika maana gani?

      15 Je, kwa kweli Musa alihitaji kurekebisha njia ya Yehova ya kufikiri? Bila shaka hapana! Ingawa Yehova alisema jambo ambalo inaelekea angefanya, huo haukuwa uamuzi wake wa mwisho. Kwa kweli, hapa Yehova alikuwa akimjaribu Musa, kama vile ambavyo baadaye Yesu alimjaribu Filipo na yule mwanamke Mgiriki. Musa alipewa nafasi ya kutoa maoni yake.b Yehova alikuwa amemchagua Musa awe mpatanishi kati Yake na Israeli, na Yehova aliheshimu uamuzi Wake wa kumweka rasmi Musa atimize daraka hilo. Je, Musa angejiacha alemewe na hisia za kukata tamaa? Je, angetumia nafasi hiyo kumhimiza Yehova asahau Israeli na kutokeza taifa lenye nguvu kutokana na wazao wa Musa mwenyewe?

  • “Ni Nani Ameijua Akili ya Yehova?”
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Oktoba 15
    • b Wasomi fulani wanasema kwamba usemi wa mfano wa Kiebrania uliotafsiriwa “niache” katika Kutoka 32:10 unaweza kuonwa kuwa mwaliko, pendekezo la kwamba Musa aruhusiwe kuingilia kati, au ‘kusimama katika mwanya,’ uliokuwapo kati ya Yehova na taifa hilo. (Zab. 106:23; Eze. 22:30) Iwe ilikuwa hivyo au hapana, bila shaka Musa alijihisi huru kumweleza Yehova maoni yake bila woga.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki