Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Israeli wa Mungu” na Ule “Umati Mkubwa”
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Julai 1
    • 8 Israeli, lilipokuwa jaminifu, lilikiri enzi kuu ya Yehova na kumkubali akiwa Mfalme. (Isaya 33:22) Hivyo, walikuwa ufalme. Lakini, kama ilivyofunuliwa baadaye, ahadi ya “ufalme” ingemaanisha mengi zaidi ya hilo. Na zaidi, walipotii Sheria ya Yehova, walikuwa safi, wakiwa wametengwa na mataifa yaliyokuwa karibu nao. Walikuwa taifa takatifu. (Kumbukumbu la Torati 7:5, 6) Je, walikuwa ufalme wa makuhani? Katika Israeli, kabila la Lawi lilikuwa limewekwa kando kwa ajili ya utumishi wa hekalu, na katika kabila hilo kulikuwa na ukuhani wa Kilawi. Sheria ya Kimusa ilipoanzishwa, wanaume Walawi walichukuliwa kwa kubadilishana na mzaliwa wa kwanza wa kila familia isiyo ya Kilawi.a (Kutoka 22:29; Hesabu 3:11-16, 40-51) Hivyo, kila familia katika Israeli ni kama iliwakilishwa katika utumishi wa hekalu. Hiyo ilikuwa kadiri ambayo taifa hilo lilipata kukaribia ukuhani. Hata hivyo, walimwakilisha Yehova mbele ya mataifa. Mgeni yeyote aliyetaka kuabudu Mungu wa kweli alipaswa kuabudu kwa kushirikiana na Israeli.—2 Mambo ya Nyakati 6:32, 33; Isaya 60:10.

  • “Israeli wa Mungu” na Ule “Umati Mkubwa”
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Julai 1
    • a Ukuhani wa Israeli ulipoanzishwa, wana-wazaliwa wa kwanza wa makabila ya Israeli yasiyo ya Kilawi na wanaume wa kabila la Lawi walihesabiwa. Kulikuwa na wazaliwa wa kwanza 273 kuliko wanaume wa Kilawi. Hivyo, Yehova akaagiza kwamba shekeli tano kwa kila mmoja wa wale 273 zilipwe zikiwa fidia kwa ajili ya ziada hilo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki