-
Jenga Itibari Katika Yehova kwa Kujifunza Neno Lake kwa Bidii-EndelevuMnara wa Mlinzi—1988 | Agosti 15
-
-
2 Hivyo Musa aliliita pamoja taifa hilo katika nyanda za Moabu zenye miinuko na vibonde. Baada ya kuipitia historia yao ya kitaifa na kurudia-rudia Sheria ya Mungu, Musa alitokeza kile ambacho kimeitwa insha yake iliyo bora zaidi. Kwa usemi wa ushairi bora kabisa, yeye alihimiza Israeli waitibari na kutii Yehova, “Mungu wa uaminifu, ambaye kwake hakuna ukosefu wa haki; mwadilifu na mnyoofu ni yeye.” Katika umalizio, Musa alihimiza hivi: “Elekezeni kabisa mioyo yenu kwenye maneno yote ambayo mimi ninanena kwa kuonya ninyi leo, kwamba ninyi mpate kuamuru wana wenu kufanya uangalifu kutenda maneno yote ya sheria hii. Kwa maana hilo si neno lisilo na thamani kwenu ninyi, bali linamaanisha uhai wenu.”—Kumbukumbu 32:4, 46, 47, NW.
‘Kuelekeza Kabisa Mioyo Yao’ Kwenye Neno la Mungu
3, 4. (a) Waisraeli walipaswa ‘kuelekeza kabisa mioyo yao’ kwenye kitu gani, na hiyo ilihusisha nini ndani? (b) Vizazi vya baadaye vilitumia shauri la Musa jinsi gani?
3 Musa aliwaonya Waisraeli kwa upole ‘waelekeze kabisa mioyo yao’ si kwenye wimbo wake wenye kusisimua tu, bali kwenye miandiko yote mitakatifu. Ilikuwa lazima wao ‘wafanye usikizi mwema’ (Knox), ‘wawe na uhakika wa kutii’ (Today’s English Version), au ‘watafakari juu ya’ (The Living Bible) Sheria ya Mungu. Ni kwa kujifahamisha nayo sana sana tu kwamba wangeweza ‘kuamuru wana wao wafanye uangalifu kutenda maneno yote ya sheria hii.’ Kwenye Kumbukumbu 6:6-8, NW, Musa aliandika hivi: “Maneno haya ambayo mimi ninaamuru wewe leo ni lazima yathibitike kuwa juu ya moyo wako; na ni lazima wewe uyakaze kikiki katika mwana wako . . . Na ni lazima wewe uyafunge yakiwa ishara juu ya mkono wako, na ni lazima yatumike kuwa kifungio cha mbele kati ya macho yako.”
-
-
Jenga Itibari Katika Yehova kwa Kujifunza Neno Lake kwa Bidii-EndelevuMnara wa Mlinzi—1988 | Agosti 15
-
-
Maandalizi ya Kujifunzia Sheria ya Mungu
6, 7. (a) Ni maandalizi gani ambayo Yehova alitoa kufanya Waisraeli wajifahamishe Sheria ya Musa? (b) Huenda ikawa pia iliwezekana jinsi gani watu wa Mungu katika nyakati za kale kuagizwa katika Neno la Mungu?
6 Ingawa hivyo, Waisraeli wangeweza jinsi gani kujifunza zile sheria-katiba za Sheria zipatazo 600? Nakala zayo bila shaka zilikuwa haba hapo kwanza. Mfalme wa wakati ujao wa Israeli alipaswa ‘kuandika katika kitabu kwa ajili yake mwenyewe nakala ya sheria hii, na ni lazima yeye asome katika hiyo siku zote za maisha yake, ili kwamba yeye apate kujifunza kuhofu Yehova Mungu wake ili kushika maneno yote ya sheria hii.’ (Kumbukumbu 17:18, 19, NW) Mungu alipanga ili Sheria hiyo isomwe kila mwezi wa saba kwenye Sikukuu ya Vibanda. (Kumbukumbu 31:10-13) Ingawa bila shaka pindi hiyo ilikuwa yenye kuburudisha, ilikuwa haitokei-tokei mara nyingi iweze kutia ndani ya watu maarifa ya kina kirefu.
7 Yehova alipanga pia kabila la Lawi liwe ‘likimwagiza Yakobo katika maamuzi ya kihukumu ya Mungu na Israeli katika sheria ya Mungu.’ (Kumbukumbu 33:8, 10; linganisha Malaki 2:7, NW.) Katika pindi fulani-fulani, Walawi waliendesha kampeni za kufundisha ambazo zilitumikia taifa zima. (2 Nyakati 17:7-9; Nehemia 8:7-9) Inaonekana kwamba, baada ya muda, angalau visehemu vya Neno la Mungu vilikuwapo pia ili watu kwa ujumla wawe navyo.a Kwa sababu hiyo, mtunga zaburi angeweza kuandika hivi: “Mwenye furaha ni mtu yule . . . [ambaye] upendezo wake ni katika sheria ya Yehova, na katika sheria yake yeye anasoma kwa sauti ya chinichini mchana na usiku.” (Zaburi 1:1, 2, NW) Hivyo himizo la Musa ‘kuelekeza kabisa mioyo yao kwenye Neno la Mungu’ lilikuwa kama amri ya kujifunza Biblia kwa bidii-endelevu.
-