Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Alikaa Macho, na Kungoja
    Igeni Imani Yao
    • 17, 18. (a) Nini kilichotukia Eliya alipokuwa njiani kuelekea Yezreeli? (b) Kwa nini inastaajabisha kuona jinsi Eliya alivyokimbia kutoka Karmeli mpaka Yezreeli? (Ona pia maelezo ya chini.)

      17 Nabii wa Yehova alianza kufuata barabara ambayo Ahabu alipitia. Ilikuwa safari ndefu katika giza na matope. Lakini jambo lisilo la kawaida likatukia.

      18 “Mkono wa Yehova ukawa juu ya Eliya, hivi kwamba akajifunga viuno, naye akakimbia mbele ya Ahabu mpaka Yezreeli.” (1 Fal. 18:46) Kwa kweli, “mkono wa Yehova” ulimwongoza Eliya kwa njia inayopita uwezo wa mwanadamu. Mji wa Yezreeli ulikuwa umbali wa kilomita 30 hivi, na Eliya hakuwa kijana.a Hebu wazia nabii huyo akiyafunga mavazi yake marefu kiunoni ili miguu yake isizuiliwe na chochote, kisha akikimbia katika barabara hiyo iliyojaa maji ya mvua kwa kasi sana hivi kwamba akalifikia gari la farasi la mfalme, akalipita, na kuliacha!

      19. (a) Nguvu na uwezo ambao Mungu alimpa Eliya unatukumbusha unabii gani? (b) Eliya alipokuwa akikimbia kwenda Yezreeli alikuwa na uhakika gani?

      19 Hiyo ilikuwa baraka kubwa kama nini kwa Eliya! Haikosi alisisimka sana kupata nguvu na uwezo huo ambao labda hata ulipita nguvu alizokuwa nazo alipokuwa kijana. Hilo linatukumbusha unabii unaowahakikishia watu waaminifu kwamba watapata afya kamilifu na nguvu katika Paradiso itakayokuwa duniani. (Soma Isaya 35:6; Luka 23:43) Eliya alipokuwa akikimbia kwenye ile barabara yenye matope, bila shaka alijua kwamba alikuwa na kibali cha Baba yake, Mungu wa pekee wa kweli, Yehova!

  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Igeni Imani Yao
    • 1, 2. Ni mambo gani yaliyotukia katika siku ya pekee maishani mwa Eliya?

      ELIYA alikimbia katika mvua huku giza likiongezeka. Ingawa hakuwa na nguvu za ujana, bado alihitaji kukimbia mwendo mrefu ili afike Yezreeli. Hata hivyo, alikimbia bila kuchoka, kwa kuwa “mkono wa Yehova” ulikuwa juu yake. Kwa kweli, hakuwa amewahi kuwa na nguvu kama hizo. Nguvu hizo zilimwezesha kuwapita farasi waliokuwa wakivuta gari la Mfalme Ahabu!​—Soma 1 Wafalme 18:46.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki