Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Igeni Imani Yao
    • 20, 21. (a) Fafanua mambo ambayo Eliya alijionea akiwa kwenye mwingilio wa pango juu ya Mlima Horebu. (b) Eliya alijifunza nini kutokana na maonyesho ya nguvu za Yehova?

      20 Yehova alishughulikiaje woga na mahangaiko ya Eliya? Malaika alimwambia Eliya asimame kwenye mlango wa pango. Alitii, bila kujua ni nini kingefuata. Ghafla, upepo wenye nguvu ukavuma! Ni lazima upepo huo ulikuwa na kelele nyingi, kwa sababu ulivuma kwa nguvu sana hivi kwamba ukapasua milima na miamba. Wazia Eliya akijaribu kukinga macho yake akiwa ameshikilia vazi lake gumu lenye manyoya, upepo huo ulipokuwa ukivuma. Alihitaji pia kusimama imara ili asianguke, kwa kuwa ardhi ilianza kutikisika, eneo hilo lilikuwa limekumbwa na tetemeko! Kabla hajaelewa kilichokuwa kikiendelea, moto mkubwa ukapita, na akalazimika kurudi ndani ya pango ili ajikinge dhidi ya joto kali.​—1 Fal. 19:11, 12.

      Elijah stands at the mouth of a cave and shields himself from the fire

      Yehova alitumia nguvu zake zisizo na kifani kumfariji na kumtia moyo Eliya

      21 Katika kila tukio, simulizi hilo linasema kwamba Yehova hakuwa katika maonyesho hayo yenye kustaajabisha ya nguvu za asili. Eliya alijua kwamba Yehova hakuwa mungu wa kuwaziwa kama Baali, aliyetukuzwa na waabudu wake waliodanganywa kwamba alikuwa “mwendeshaji wa mawingu,” au mleta-mvua. Yehova ndiye Chanzo halisi cha nguvu zote za asili zisizo na kifani, lakini pia ni mkuu kuliko kitu chochote alichoumba. Hata mbingu haziwezi kumtosha! (1 Fal. 8:27) Mambo hayo yote yalimsaidiaje Eliya? Kumbuka alikuwa na woga. Kwa vile Yehova Mungu mwenye nguvu nyingi sana alikuwa upande wake, Eliya hakupaswa kuwaogopa Ahabu na Yezebeli!​—Soma Zaburi 118:6.

      22. (a) Ile “sauti tulivu, ya chini” ilimhakikishiaje Eliya kwamba alikuwa mwenye thamani? (b) Huenda ni nani aliyekuwa chanzo cha ile “sauti tulivu, ya chini”? (Ona maelezo ya chini.)

      22 Baada ya moto kupita, kimya kikatokea na Eliya akasikia “sauti tulivu, ya chini.” Ilimwomba ajieleze tena, naye akafanya hivyo, akieleza mahangaiko yake yote kwa mara ya pili.a Labda hilo lilimtuliza. Bila shaka, Eliya alitulizwa hata zaidi na maneno ambayo ile “sauti tulivu, ya chini” iliongezea. Yehova alimhakikishia Eliya kwamba alikuwa mwenye thamani sana. Jinsi gani? Mungu alimfunulia mengi kuhusu makusudi yake ya wakati ujao ya kuangamiza ibada ya Baali katika Israeli. Ni wazi kwamba kazi ya Eliya haikuwa ya bure, kwa kuwa bado Mungu angetimiza makusudi yake. Zaidi ya hayo, Eliya alihusika katika kutimiza makusudi hayo, kwa kuwa Yehova alimtuma na kumpa maagizo hususa.​—1 Fal. 19:12-17.

  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Igeni Imani Yao
    • a Huenda ile “sauti tulivu, ya chini” ilikuwa ya malaika aliyetumiwa kupeleka “neno la Yehova” anayetajwa katika 1 Wafalme 19:9. Katika mstari wa 15 malaika huyo anatajwa kama “Yehova.” Huenda tukakumbuka mjumbe wa Yehova aliyetumiwa kuwaongoza Waisraeli nyikani na ambaye Mungu alisema hivi kumhusu: “Jina langu limo ndani yake.” (Kut. 23:21) Bila shaka, hatuwezi kusema jambo hili kwa uhakika, lakini tunapaswa kukumbuka kwamba kabla ya kuja duniani, Yesu alikuwa “Neno,” Msemaji maalumu wa Yehova kwa watumishi wake.—Yoh. 1:1.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki